Kijana Samson Peter mtuhumiwa wa utekaji wa watoto, Afariki kwa kupigwa risasi na Polisi akijaribu kutoroka..#share
KIJANA anayetuhumiwa kwa kosa la utekaji wa watoto jijini Arusha,
Samson Peter amefariki dunia kwa kupigwa risasi na askari polisi akijaribu
kuwakimbia wakati wapo njiani kwenda kuwaonyesha washirika wenzake wa utekaji katika
eneo la Muriet Mkoni jijini humo.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha Charles Mkumbo amethibitisha
kutokea kwa kifo hicho na kubainisha kwamba
mtuhumiwa huyo alipigwa risasi ya mguuni kama onyo la kujaribu kumtoroka
Askari aliyekuwa ameongozana naye majira hayo ya saa 5:30 usiku.
Mkumbo amesema kuwa baada ya tukio hilo la kumjeruhi
mtuhumiwa Samson Peter kwa nia ya kumuadhibu, alifikishwa Hospital ya Mt. Meru ili
kupatiwa matibabu lakini alifariki kutokana na kuvuja damu.
"Ni kweli mtuhumiwa amefariki. Ambapo jana usiku wakati
alipokuwa amesindikizwa na polisi kuwaonyesha waashirika wenzake alitaka
kutoroka, lakini katika hatua ya kumuadhibu kwa kitendo chake hicho ndipo
akapigwa risasi ya mguuni ambapo ilimpelekea kuvuja damu nyingi na alifariki
baada ya kufikishwa hospitali" amesema Kamanda Mkumbo.
Hata hivyo Kamanda Mkumbo amesema msako zaidi wa kuunasa
mtandao huo bado unaendelea na iwapo wakipatikana wote watakumbana na mkono wa
sheria.
Na Mwandishi Wetu





No comments:
Post a Comment