Breaking News: Mwanasheria Mkuu Chadema Tundu Lissu apigwa risasi....#share
Tundu Lissu amepigwa risasi.
Chanzo:Mbunge Marwa Ryoba wa Serengeti kupitia ukrasa wake wa facebook, amsema kuwa Mbunge wa Singida Mashariki na Mwanasheria Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) amepigwa Risasi.
Lakini hajaeleza chanzo cha kupigwa kwake "Lissu amepigwa risasi" ameandika
Aidha Mwenyekiti wa Chadema Freeman
Mbowe amethibitisha kutokea kwa tukio hilo la kupigwa risasi kwa
Mwanasheria Mkuu wa chama hicho Tundu Lissu akiwa nyumbani kwake mjini Dodoma.
Amesema kwa sasa Lissu amepelekwa
katika hospitali ya Mkoa wa Dodoma kwa ajili ya kupatia matibabu huku akieleza
hali yake kuwa mbaya sana.
“Ni kweli amepigwa risasi akiwa
nyumbani kwake, na sasa yupo katika hospitali ya mkoa Dodoma, naomba uniache
kwa sasa,” amesema Mbowe akiongea na ITV mda mfupi uliopita.
Na Abraham Ntambara
Na Abraham Ntambara





No comments:
Post a Comment