MAHAKAMANI KISUTU: Mfanyabiashara Yusuf Manji aibwaga serikali ya JPM... Aishi Keko kwa miezi...#share
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu imeamuachia huru
mfanyabiashara Yusuf Manji katika kesi ya uhujumu uchumi baada ya Mkurugenzi
Mkuu Mashtaka (DPP) kuwasilisha hati akionyesha kutokuwa na nia ya kuendelea na
mashtaka dhidi ya Manji na wenzake.

Mwenyekiti huyo wzamani wa Klabu ya Yanga na wenzake watatu walikuwa
wakikabiliwa na mashtaka saba yakiwemo ya uhujumu uchumi, kukutwa na mihuri
miwili ya JWTZ, ukiwemo wa Mkuu wa Kikosi cha 21 JWTZ, wa Mkuu wa Kikosi
Makutupora Dodoma (JWTZ) na wa Commanding Officer Korogwe na plate number mbili
za magari ya serikali.
Watuhumiwa wengine walioachiwa huru kwenye kesi hiyo ni
Deogratius Kasinda na Thobias Pwere na mwingine.
Kuachiwa huru kwa Manji dhidi ya kesi hiyo ni kwamba sasa
atabaki akikabiliwa na kesi moja tu ya matumizi ya dawa za kulevya ambayo bado
iko mahakamani.
Aidha kuondolewa kwa kesi hiyo kumekuja siku moja baada ya
Mfanyabiashara huyo kuporwa na Serikali ardhi ya ekali 712 eneo la Kigamboni
Jijini Dar es Salaam.
Unaweza kusema Manji amekuwa katika misukosuko kwa muda mrefu
hadi kufikia hatua ya kuishi katika gerezani.
Na Mwandishi wetu



No comments:
Post a Comment