Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan Awataka Majaji na Mahakimu Kupambana na Rushwa...Habari Kamili Hii Hapa na Matukio360..#share

MAKAMU wa Rais Samia Suluhu Hassan amewataka Majaji na Mahakimu kupambana na rushwa katika mahakama ili kuhakikisha haki na maendeleo vinapatikana.


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan akizungumza katika ufunguzi wa Mkutano wa Mwaka wa chama cha majaji na mahakimu wa Jumuiya ya Madola unaofanyika jijini Dar es Salaam kwa siku tatu mfurulizo ambapo kauli mbiu ya Mkutano huo ni  'Mahakama Madhubuti, inayowajibika na Jumuishi'.Mkutano huo umehudhuriwa na majaji pamoja na mahakimu wa nje mwanachama wa Jumuiya ya Madola.


Kauli hiyo ameitoa leo jijini Dar es Salaam wakati akifungua Mkutano mwaka wa siku tatu wa Majaji  na Mahakimu wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Madola jijini Dar es Salaam kwa niaba ya  Rais  John Magufuli.

Aidha amesema kuwa rushwa huondoa uhuru wa mahakama na hivyo kupoteza utawala wa sharia.

“Niwatake washiriki wa mkutano huo kupambana na rushwa katika mahakama ili kuhakikisha haki na maendeleo vinapatikana,” amesema Makamu wa Rais.

Makamu wa Rais amepongeza mafanikio makubwa yaliyofikiwa na Chama cha Majaji na Mahakimu wa nchi wananchama wa Jumuiya ya Madola (CMJA).

Amesema ” Jitihada zenu katika kuendeleza na kuimarisha viwango na uhuru wa mahakama na vilevile kuendeleza utawala wa sheria vimeendelea kuimarika na kuifanya jumuiya yenu kuwa imara zaidi”.

“Kwa miaka mingi mmeendelea kuchochea na kuimarisha uhuru wa mahakama huku mkijitahidi kuendeleza utawala wa sheria katika nchi za jumuiya ya madola,” amesema Makamu wa Rais.

Aidha, mkutano huo uliohudhuriwa na Majaji Wakuu wa Mahakama, majaji na mahakimu, Makamu wa Rais aliuasa mhimili wa Mahakama kuunga mkono jitihada za serikali katika mapambano ya kuondoa umaskini na rushwa ili kufikia maendeleo ya kweli. “Naamini kwamba nia ya kujenga mahakama yenye ufanisi, uwajibikaji na jumuishi haitafikiwa kama mahakama ya Tanzania itajitenga na jitihada za serikali za kuondoa umaskini na rushwa”, alisisitiza Makamu wa Rais.

Amewahakikishia washiriki wa mkutano huo kwamba serikali ya Tanzania itaendelea kuheshimu na kuimarisha uhuru wa Mahakama kwa  kuhakikisha inaendelea kupambana na kuondoa vitendo vya rushwa. 

Akizungumza na waandishi wa habari baada ya ufunguzi wa mkutano huo, Rais wa Chama cha Majaji na Mahakimu Tanzania, Ignasi Kitasi amesema moja ya changamoto inayowakabili ni ufinyu wa bajeti inayoelekezwa kwenye shughuli za mahakama unachangia kukwamisha utoaji huduma na utendaji wa mahakama katika kusguhulikia mashauri mabalimbali.
Rais wa Chama cha Majaji na Mahakimu Tanzania, Ignasi Kitasi akizungumza na waandishi wa habari baada ya ufunguzi wa mkutano wa siku tatu wa Majaji na Mahakimu wa Nchi za Jumuiya ya Madora leo Jijini Dar es Salaam (Picha na Abraham Ntambara)

Amesema kutokana ufinyu wa rasilimali fedha mahakama zimekuwa zikishindwa kukamilisha majukumu yake kwa wakati mwafaka huku akisisitiza ufinyu huo husababisha malalamiko kutoka kwa wananchi wenye madai na kesi ambazo ziko mahakamani.

" Changamoto kubwa inayoikabili mahakama bdao bajeti inayotengwa ni finyu tatizo hili linapelekea shughuli za utendaji kutofanyika ipasavyo likiwekewa mkazo naamini malalamiko yatapungua," amesema Kitasi.

Amefafanua kuwa mahakama nchini zinaendelea kufanya kazi bila kuingiliwa huku akiongeza mkutano huo umebeba kauli mbiu inayohimiza kujenga mahakama shirikisha inayowajibika.

Jaji Mkuu, Profesa Ibrahim Juma  akizungumza katika Mkutano wa Mwaka wa chama cha majaji na mahakimu wa Jumuiya ya Madola  unaofanyika Dar es Salaam kwa siku tatu Mfurulizo Mkutano huo unakauli mbiu inayosema  'Mahakama Madhubuti, inayowajibika na Jumuishi'.


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan akiwa katika picha ya pamoja na Majaji pamoja na mahakimu wanawake waliohudhuria mkutano Mkuu wa Mwaka wa Majaji na mahakimu wa Jumuiya ya Madola Unaofanyika jijini Dar es Salaam.



Na Hussein Ndubikile



About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search