Meya Jacob Abaini Mchezo Mchafu Sakata la Vyeti Feki vya "Bashite"...Soma Habari Kamili na Matukio360..#share
TUME ya Maadili ya Viongozi wa Umma, inatarajia kumhoji
Meya wa Manispaa ya Ubungo, Boniface Jacob kuhusu madai yake
aliyowasilisha kwa tume hiyo akitaka Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul
Makonda kwamba ameghushi vyeti vya shule.

Jacob amesema kuwa tume hiyo imemtaka afike ofisini kwao
kesho asubuhi ili aweze kutoa maelezo juu ya mashtaka yake juu ya Makonda.
Meya huyo ambaye pia ni Diwani wa
Ubungo amesema ameitwa kupitia barua yenye kumbukumbu namba CAG
31/37/01/42.
Hata hivyo, Jacob amesema kuwa tayari kuna viashiria vya
vishawishi vya yeye kuachana na shauri hilo linalomkabili Makonda.
Mwezi Machi mwaka huu Jacob aliwasilisha mashtaka manne
katika tume hiyo pamoja na moja la jinai ambalo ni la kughushi
vyeti vya taaluma.
Hivi karibuni Makonda alipachikwa jina la Bashite ambalo
linadaiwa ndilo jina lake halisi alilopewa na wazazi wake.
Na Mwandishi Wetu
No comments:
Post a Comment