Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Jenerali Venance Mabeyo awaonya Chadema kugeuza mtaji wa kisiasa shambulio la Tundu Lissu.. #share

MKUU wa majeshi ya Ulinizi na Usalama nchini Jenerali Venance Mabeyo ameshtushwa na namna Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) wananvyoweka uzito mkubwa katika tukio la kushambuliwa kwa Tundu lissu.


Jenerali Mabeyo ametoa kauli hiyo leo jijini Dar es Salaam akizungumza na waandishi wa habari, amesema kitendo cha kupigwa risasi Rais huyo wa Chama cha Mawakili Tanganyika (TLS) limefanywa kuwa tukio kubwa kuwahi kutokea  wakati kuna matukio makubwa  kama ya Kibiti ambayo yaliyoathiri na kuua watu wengi  na vyombo vya usalama viliachwa kufanya kazi yao.

‘kwanini matukio ya kibiti hayaleti mstuko mkubwa sana sasa wakati watu walioathirika ni wengi zaidi kuliko matukio ya sasa?’ amehoji Jenerali mabeyo.

Aidha Jenerali Mabeyo amewataka wananchi kuwa watulivu na kuviacha vyombo vya dola kufanya kazi yake kwani kwa sasa  vimeingia kazini.

Mkuu huyo wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama ameahidi kuwa wahusika wote watawatia nguvuni  na hali itakuwa shwari.

Na Mwandishi Watu

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search