Zitto Kabwe akwama tena kwa Spika Ndugai,.. “tutakwenda sambamba mguu kwa mguu hadi kieleweke.." #share
MBUNGE wa Kigoma Mjini
(ACT-Wazalendo), Zitto Kabwe
amemjibu Spika Job Ndugai kuwa
ameibua mashitaka yake ili kufunika ufuatiliaji wa wananchi
kuhusu hali ya Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu.
Zitto aliandika majibu hayo
jana mchana muda mchache
baada ya Spika Ndugai kueleza
kuwa anaweza kumzuia kuzungumza bungeni kwa muda wote uliobaki.
Alibainisha kuwa amegundua
Ndugai ameibua mashitaka dhidi
yake, ili kufunika ufuatiliaji wa
wananchi kuhusu Lissu kupigwa
risasi.
Jana asubuhi bungeni Dodoma,
Spika Ndugai alisema anaweza
kumpiga marufuku Zitto kuzungumza bungeni kwa kipindi chote cha Bunge la 11 na hana cha
kumfanya.
Spika alitoa kauli hiyo siku
moja tangu alipompeleka Zitto
kwenye Kamati ya Haki, Kinga
na Madaraka ya Bunge kwa kudharau Bunge.
Akizungumza jana baada ya
kipindi cha maswali na majibu,
Ndugai alisema anaweza kulichambua Bunge, kwa sababu
alikuwapo katika vipindi hivyo,
na Anne Makinda na marehemu
Samwel Sitta ni walimu wake.
“Hawa ni watu nawaheshimu
sana na wamenilea sana na mpaka sehemu nilipofika leo. Utanilinganishaje mimi na milima mikubwa kama Kilimanjaro? Hata
siku moja, sikio haliwezi kuzidi
sikio,” alisema.
Alibainisha kuwa katika Bunge
la Tisa, Zitto alipeleka hoja ya
Mgodi wa Buzwagi ambayo
ilikataliwa na Bunge, lakini ikazuka hoja ya kimaadili na alihukumiwa hapo hapo.
“Alihukumiwa hapo hapo akapigwa miezi mitatu. Mnataka
niende mkuku kama Bunge la
Tisa nifanane na Mzee Sitta? Hilo
pia naliweza kwa nini mnaalika
matatizo, nashangaa unapambana na Spika,” alisema.
Alisema ana uwezo wa kupiga
marufuku kuzungumza hadi
miaka yote mitano na Mbunge
huyo wa Kigoma Mjini, akose pa
kuongelea na hakuna swali lolote
atakalouliza na kumtaka kupambana na watu wengine, lakini si yeye.
“Kwa haya ya Spika sina sababu
nayo, lakini ya kulidharau Bunge
hayo sitayavumilia, nitalinda
mhimili huu kwa nguvu zangu
zote,” alisema.
Alisisitiza hawawezi kuacha
wabunge kulidhalilisha Bunge na
kuhoji watachukuliaje Watanzania wengine watakapolidhalilisha Bunge.
Alisema kwa kuwa hilo ni kosa
la pili kwa Zitto, ameagiza apelekwe katika Kamati ya Maadili,
“tutakwenda sambamba mguu
kwa mguu hadi kieleweke.”
(ACT-Wazalendo), Zitto Kabwe
amemjibu Spika Job Ndugai kuwa
ameibua mashitaka yake ili kufunika ufuatiliaji wa wananchi
kuhusu hali ya Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu.
Zitto aliandika majibu hayo
jana mchana muda mchache
baada ya Spika Ndugai kueleza
kuwa anaweza kumzuia kuzungumza bungeni kwa muda wote uliobaki.
Alibainisha kuwa amegundua
Ndugai ameibua mashitaka dhidi
yake, ili kufunika ufuatiliaji wa
wananchi kuhusu Lissu kupigwa
risasi.
Jana asubuhi bungeni Dodoma,
Spika Ndugai alisema anaweza
kumpiga marufuku Zitto kuzungumza bungeni kwa kipindi chote cha Bunge la 11 na hana cha
kumfanya.
Spika alitoa kauli hiyo siku
moja tangu alipompeleka Zitto
kwenye Kamati ya Haki, Kinga
na Madaraka ya Bunge kwa kudharau Bunge.
Akizungumza jana baada ya
kipindi cha maswali na majibu,
Ndugai alisema anaweza kulichambua Bunge, kwa sababu
alikuwapo katika vipindi hivyo,
na Anne Makinda na marehemu
Samwel Sitta ni walimu wake.
“Hawa ni watu nawaheshimu
sana na wamenilea sana na mpaka sehemu nilipofika leo. Utanilinganishaje mimi na milima mikubwa kama Kilimanjaro? Hata
siku moja, sikio haliwezi kuzidi
sikio,” alisema.
Alibainisha kuwa katika Bunge
la Tisa, Zitto alipeleka hoja ya
Mgodi wa Buzwagi ambayo
ilikataliwa na Bunge, lakini ikazuka hoja ya kimaadili na alihukumiwa hapo hapo.
“Alihukumiwa hapo hapo akapigwa miezi mitatu. Mnataka
niende mkuku kama Bunge la
Tisa nifanane na Mzee Sitta? Hilo
pia naliweza kwa nini mnaalika
matatizo, nashangaa unapambana na Spika,” alisema.
Alisema ana uwezo wa kupiga
marufuku kuzungumza hadi
miaka yote mitano na Mbunge
huyo wa Kigoma Mjini, akose pa
kuongelea na hakuna swali lolote
atakalouliza na kumtaka kupambana na watu wengine, lakini si yeye.
“Kwa haya ya Spika sina sababu
nayo, lakini ya kulidharau Bunge
hayo sitayavumilia, nitalinda
mhimili huu kwa nguvu zangu
zote,” alisema.
Alisisitiza hawawezi kuacha
wabunge kulidhalilisha Bunge na
kuhoji watachukuliaje Watanzania wengine watakapolidhalilisha Bunge.
Alisema kwa kuwa hilo ni kosa
la pili kwa Zitto, ameagiza apelekwe katika Kamati ya Maadili,
“tutakwenda sambamba mguu
kwa mguu hadi kieleweke.”




No comments:
Post a Comment