Mshambuliaji wa Everton Wayne Rooney kukumbana na Rungu la Koeman kwa Utovu wa nidhamu..#share

WAYNE Rooney atakutana na mgogoro mkubwa atakapokutana na kocha wake  Ronald Koeman wiki hii na huenda akakabiliwa na adhabu kutoka kwa meneja huyo.


Nahodha huyo wazamani Uingereza alipewa onyo kabla ya kujiunga kwa mara nyingine na klabu ya  Everton kwa kuambiwa na Koeman kuwa ni lazima kwa kila mchezaji wake kuishi nidhamu.

Lakini Rooney, ambaye alikamatwa na polisi ijumaa iliyopita kwa kumuendesha mtoto wa kike nyumbani kwake huku akiwa amelewa atajumuishwa  katika kikosi kwa kuwa kocha alishindwa kusajili mshambuliaji mwingine wa kati katika dirisha lililofungwa.

Ukweli ni kwamba Koeman kwa sasa anamuhitaji Rooney, hususani katika michezo ya lighi ya  Europa inayokuja.

Koeman alizungumzia maswala ya pombe katika mkutano mrefu na Rooney kabla ya kumsaini, baada ya kuonya juu ya matukio yanayohusiana na kunywa pombe ambayo yamepunguza ubora wa kiwango chake.

Koeman alihakikishiwa na mshambuliaji huyo wa zamani wa timu ya Manchester United kuwa hatarudia tabia hiyo ya ulevi.

Pamoja na tabia hiyo ya Rooney ni ukweli kwamba meneja wake anavutiwa na mtazamo wa mchezaji na jinsi anavyojituma katika mazoezi na  wakati wa mechi.


Kama Rooney atapewa adhabu na Koeman hatakuwa mchezaji wa kwanza kuadhibiwa na kinidhamu na Meneja huyo kwani wliowahi kupewa adhabu ni pamoja na Zlatan Ibrahimovic akiwa Ajax and Santiago Canizares akiwa Valencia.


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search