Siku Kadhaa Baada ya Kuachiwa Huru Mfanyabiashara Yusuf Manji Ameripoti Tena Mahakamani Leo....#share
KESI ya matumizi ya dawa za kulevya inayomkabili Mfanyabiashara Yusuf Manji inatarajiwa kusikilizwa kwa siku tatu mfululizo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam.
Hivyo kesi hiyo itaanza kusikilizwa kuanzia Septemba 25 hadi 27 mwaka huu kwa kusikiliza ushahidi wa upande wa utetezi wa Mfanyabiashara huyo.
Wakili wa Serikali Mkuu, Timony Vitalis amemueleza Hakimu Mkazi Mfawidhi, Cyprian Mkeha kuwa, kesi hiyo imeitishwa kwa ajili ya kuendelea na ushahidi lakini yeye ana safari akidai kuwa leo mchana anatarajia kusafiri, hivyo ushahidi wa kesi hiyo ukianza kusikilizwa atachelewa.
Baada ya kueleza hayo, Hakimu Mkeha alimuuliza Manji kwa nini amechelewa kufika Mahakamani, ambapo Manji alijibu alikuwa eneo la karibu hivyo alisubiri aitwe na Wakili wake.
"Nisamehe sana Mheshimiwa, niliambiwa umetoka, hivyo nilisubiri Wakili anipigie simu kama ungerudi,"
Baada ya kueleza hayo, Hakimu Mkeha aliahirisha kesi hiyo hadi September 25-27, 2017 kwa ajili ya kusikilizwa mfululizo.
Hivyo kesi hiyo itaanza kusikilizwa kuanzia Septemba 25 hadi 27 mwaka huu kwa kusikiliza ushahidi wa upande wa utetezi wa Mfanyabiashara huyo.
Wakili wa Serikali Mkuu, Timony Vitalis amemueleza Hakimu Mkazi Mfawidhi, Cyprian Mkeha kuwa, kesi hiyo imeitishwa kwa ajili ya kuendelea na ushahidi lakini yeye ana safari akidai kuwa leo mchana anatarajia kusafiri, hivyo ushahidi wa kesi hiyo ukianza kusikilizwa atachelewa.
Baada ya kueleza hayo, Hakimu Mkeha alimuuliza Manji kwa nini amechelewa kufika Mahakamani, ambapo Manji alijibu alikuwa eneo la karibu hivyo alisubiri aitwe na Wakili wake.
"Nisamehe sana Mheshimiwa, niliambiwa umetoka, hivyo nilisubiri Wakili anipigie simu kama ungerudi,"
Baada ya kueleza hayo, Hakimu Mkeha aliahirisha kesi hiyo hadi September 25-27, 2017 kwa ajili ya kusikilizwa mfululizo.
No comments:
Post a Comment