TMA imetoa leo mwelekeo wa mvua kwa kipindi cha mwezi Oktoba hadi Disemba...Pia imezitaka sekta zinazohusika na hali ya hewa....#share
MAMLAKA ya Hali ya Hewa nchini (TMA) imetoa mwelekeo wa mvua
za vuli na mifumo ya hali hiyo katika
kipindi cha mwezi Oktoba hadi Disemba mwaka huu na athari zake huku ikizitaka
sekta mbalimbali zinazohusiana na hali ya hewa kujiandaa kutelekeza majukumu yake.
Sekta hizo ni kilimo na usalama wa chakula, mifugo na
wanyamapori, maliasili na utalii, nishati na maji, mamlaka za miji, afya na
Menejimenti za maafa.
Hayo yamesemwa leo jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi Mkuu wa
TMA, Dk Agnes Kijazi wakati akizungumza na wanahabari kuhusiana na mvua hizo.
Amebainisha kuwa katika kipindi hicho mvua zinatarajiwa kuwa
za wastani katika maeneno mengi ya mikao ya Kagera, Mara, Mwanza, Geita, Dar es
Salaam, Kilimanjaro na Arusha huku akisistiza utabiri wa maeneo mengine
yaliyosalia utatolewa mwezi Oktoba.
''Mvua za chi ya
wastani na vipindi virefu vya ukavu vinatarajiwa kujitokeza hususan
katika mikoa iliyotajwa pamoja na maeneo ya Visiwa vya Unguja na Pemba,'' amesema
Dk. Kijazi.
Dk Kijazi amesema kuanzia mwezi Septemba hadi Oktoba maeneo
ya Ziwa Viktoria, ukanda wa pwani yatapata mvua za vuli na kwamba Novemba
Nyanda za Juu Kaskazini Masahariki mvua zitanyesha eneo hilo.
Ameongeza kuwa ongezeko la mvua linatarajiwa katika miezi ya
Novemba na Disemba ikiendana na vipindi virefu vya ukavu vikitarajiwa
kujitokeza Oktoba.
Amefafanua kuwa mvua hizo kanda ya ziwa mvua hizo zitaanza
maapema kati ya wiki ya pili na tatu ya Septemba na kusambaa katika mikoa ya
Geita, Shinyanga, ifikapo wiki ya tatu
na ya nne ya mwezi huo huku zikitarajiwa kuisha wiki ya nne ya mwezi Disemba.
Pia amesema Nyanda za juu kaskazini Mashariki mvua hizo
zitaanza wiki ya pili na ya tau ya mwezi
Novemba zikitarajiwa kuwa za wastani hadi juu ya wastani akibainisha zitaisha
wiki ya nne ya mwezi Disemba.
Dk. Kijazi amesema hali ya joto la juu ya wastani iliyopo
magharibi mwa Bahari ya Hindi inatarajiwa kuendelea katika kipindi cha mwezi
Oktoba hadi Disemba.
Amewashauri wakulima na wafugaji kuvuna maji kwa ajili ya
matumizi ya baadaye pamoja na wachimbaji madini kuwa makini na ongezeko la maji
linaloweza kusababisha maporomoko.
Aidha, amezishauri mamlaka hizo kuhakikisha mifumo ya maji
inafanya kazi ipasavyo ili kupeusha maji kutuama na kwamba wananchi
wameshauriwa kujikinga na magonjwa ya milipuko.
Katika hatua nyingine ameishauri menejimenti hiyo kuhakikisha
inatunza mazingira, matumizi mazuri ya ardhi na mipango miji pamoja na
maandalizi hatua stahiki zinazotakiwa kuchukuliwa kutokana na madhara ya mvua.
Na Hussein Ndubikile




No comments:
Post a Comment