Waziri Nchemba Awajibu Chadema Kuhusu Vyombo vya Nje kufanya Uchunguzi Shambulio la Lissu..Habari Kamili Hii Hapa na Matukio360..#share

WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mwigulu Nchemba amesema kuwa watu wanaofanya uhalifu dakika zao zinahesabika kwani Serikali imejipanga kuhakikisha inalinda usalama wa Wananchi.
Kauli hiyo amekuja siku kadhaa baada ya kuibuka kwa matukio mbalimbali ya uhalifu nchini kwa baadhi ya watu kushambuliwa kwa risasi akiwemo Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu na taarifa zikidai wahalifu hao hawajulikani.

Akizungumza na wananchi wa Kata ya Kinampanda wilaya ya Iramba mkoani Singida  leo waziri Nchemba amewataka wananchi kuwa na amani  kwani anaimani kubwa na vyombo vya ulinzi na usalama nchini katika kulinda raia na mali zao.

“Mimi ndiye niliyepewa dhamana ya usalama wa raia na mali zao katika wizara ya mambo ya ndani basi hapatatokea hata kakitongoji kamoja au kauchochoro ambacho kitaonekana kimeshindikana ndani ya nchi yetu,”amesema Nchemba.


Waziri Nchemba ameongeza kuwa nchi hii ni nchi huru ambayo inajitegemea na kuna watu wanasema wanataka vyombo vya nje vifanye uchunguzi, hawa watu wanao fanya uhalifu nchini, upelelezi utafanywa na watu wetu, watakamatwa na vyombo vyetu na watafikishwa katika vyombo vya sheria vya hapahapa  tunatakiwa kuamini vyombo vyetu, kama serikali tutashugulikano kwelikweli na si kama hatujaanza nao tunashughulika nao.

Na Mwandishi Wetu

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search