Yaliyojiri Kisutu Leo: Wakili Mutalemwa amuweka pabaya Halima Mdee kesi ya kumtusi Rais... Hakimu Nongwa apeleka October 11.. #share

Upande wa mashtaka katika kesi ya kumtolea lugha ya matusi Rais John Magufuli inayomkabili, Mbunge wa Kawe, Halima Mdee umeieleza mahakama ya hakimu Mkazi Kisutu kuwa, upelelezi wa kesi hiyo umekamilika.

Wakili wa serikali mwandamizi, Mutalemwa Kishenyi amemueleza Hakimu Mkazi Mkuu, Victoria Nongwa, leo kuwa upelelezi wa kesi hiyo umekamilika.

Kishenyi amedai kuwa anaiomba mahakama hiyo, ipange tarehe kwa ajili ya kumsomea mshtakiwa maelezo ya awali (PH).

Baada ya kusema hayo, wakili wa Mdee, Peter Kibatala alidai kuwa wanaondoa mapingamizi yao ya kwamba mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza kesi hiyo.

Baada ya kuelezwa hayo, Hakimu Nongwa aliahirisha kesi hiyo hadi October 11/2017 kwa ajili ya mshtakiwa kusomewa maelezo ya awali.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search