ACT-Wazalendo wampa neno Magufuli...soma habari kamili na Matukio360...#share

Na Mwandishi Wetu 

CHAMA  cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali ya Tanzania, Jumuiya ya Afrika Mashariki, Umoja wa Afrika na Jumuiya za kimataifa kuendelea na juhudi za kuleta amani nchini Somalia.
Kiongozi Mkuu wa ACT-Wazalendo Zitto Kabwe

Kauli hiyo imekuja baada ya kutokea kwa vifo vya watu zaidi ya 250 kutokana na mlipuko wa mabomu uliotokea ndani ya Lori mjini Mogadishu nchini Somalia.

Taarifa iliyotolewa leo na Mwenyekiti kamati ya mambo ya nje na ushirikiano wa Kimataifa wa ACT Venance Msebo amesema chama hicho kimepokea kwa masikitiko makubwa taarifa ya vifo vya watu hao.

Aidha mbali na vifo hivyo, watu zaidi ya 400 wamejeruhiwa katika tukio hilo. Shambulio hilo linadaiwa kutekelezwa na kikundi cha kigaidi cha Al-Shabab usiku wa Oktoba 14 mwaka huu.

“Inasikitisha sana kuona maisha ya mamia ya watu yakikatizwa kinyama namna hiyo, wakati viongozi, wananchi na taasisi mbalimbali duniani wakifanya juhudi kuhakikisha dunia inakuwa sehemu salama ya kuishi inahuzunisha kushuhudia matukio ya kidhalimu kama hayo yakiendelea kutukia,” amesema Msebo .

“Tunatoa pole kwa serikali na wananchi wa Somalia, tunawaombea kwa Mwenyezi Mungu awajalie uvumilivu na ustahimilivu katika kipindi hiki kigumu cha kuondokewa na mamia ya ndugu zao,”.

Ameeleza kwamba juhudi za makusudi zinapaswa kuchukuliwa ili kuepusha maafa na madhara zaidi yanayoweza kusababishwa na kutokuwepo usalama nchini humo. Somalia isipokuwa salama Afrika haiwezi kuwa salama, bila Somalia salama hakuna dunia salama.



About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search