Askofu Shao: Magufuli kama Mugabe..Soma habari kamili na Matukio360..#share

Na Abraham Ntambara

ASKOFU wa Jimbo Katoliki la Zanzibar Mhashamu Agustino Shao amemfananisha Rais John Magufuli na Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe kwa jinsi anavyochukua hatua katika kupigania maslahi ya Watanzania.
Rais John Magufuli (Kulia) na Rais Robert Mugabe (Kushoto)

Taarifa iliyotolewa leo kwa vyombo vya habari na Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu, imesema, Askofu Shao amesema hayo wakati akihubiri katika Misa Takatifu iliyofanyika katika Kanisa Katoliki la Mtakatifu Joseph, Porokia ya Minaramiwili, amesema Rais Mugabe alichukua hatua za kupigania maslahi ya Wazimbabwe na sasa wananachi wa nchi hiyo wameanza kuzalisha bidhaa na kuziuza nje ya nchi.


Hivyo Askofu Shao amesema hatua anazochukua Rais Magufuli kupambana na rushwa, kupigania rasilimali za Watanzania, kuimarisha nidhamu na uwajibikaji, kukabiliana na wizi na ubadhilifu wa mali za umma na kubana matumizi zinapaswa kuungwa mkono na watanzania wote. 

"Hatuwezi kusema tunaimaliza rushwa wakati tunaendelea kuishi kwa kupata fedha ambazo hujazifanyia kazi, ni lazima tuishi machungu ya kuimaliza rushwa, ni lazima tuishi machungu ya kuweka uadilifu katika utendaji wetu, tusipoishi machungu hayo tutaishi dunia mbili, dunia ya rushwa na dunia ya kujenga uchumi na uadilifu wa watanzania, tukubali kujikatalia ili tuweze kupata mazuri tuliyotaka," amesema Askofu Shao.

Kwa upende wake Rais Magufuli amemshukuru Askofu Shao kwa mahubiri yake mazuri ambapo ameungana naye katika kuwahakikishia Watanaznia kuwa Serikali inachukua hatua za kupambana na rushwa na kulinda rasilimali za nchi ili ziweze kuwanufaisha wenyewe.




[​IMG]

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search