Aliyeua wanafunzi watano auawa...Soma habari kamili na Matukio360..#share

MTU mmja anayetuhumiwa kwa mauaji ya wanafunzi watano na mlinzi mmoja katika shule ya Sekondari ya Lokichogio huko Turkana nchini Kenya ameuawa na wakazi wa kambi ya wakimbizi ya Kakuma.



Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta

Mtuhumiwa huyo alikuwa amekamatwa na polisi kabla ya wakazi hao kuvamia Kituo cha Polisi cha Kakuma na kumchoma moto.

Kamanda wa Polisi wa Turkana Ronad Opili amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema mtu huyo alikamatwa kwenye kambi ya wakimbizi ya Kakuma alipokuwa akijaribu kukimbilia Sudan Kusini.

"Wanafunzi kadhaa wamejeruhiwa. Hatuwezi kuthibitisha idadi yao hadi tupate taarifa za hospitali,” amesema Kamanda Opili akizungumza na waandishi wa habari.


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search