Serikali kuanzisha operesheni maalum kudhibiti uchafu...soma habari kamili na Matukio360..#share
Na
Hussein Ndubukile
SERIKALI
imesema kuanzia Novemba Mosi hadi Disemba 31,2017 itaendesha oparesheni maalum
ya kudhibiti uchafuzi wa mazingira nchini kwa lengo lakukabiliana na madhara
yatokanayo na mvua.
Hayo
yamesemwa leo jijini Dar es Salaam na Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa
Rais, Muungano na Mazingira, Kange Lugola wakati alipotembea eneo la Tandale
kwa Mtogole wilayani Kinondoni ambalo limeathirika na Mafuriko.
Amesema
tatizo la mafuriko katika eneo hilo na maeneo mengine ya nchi yanachangiwa na
uchafuzi wa mazingira unaosababishwa na takataka zinazotupwa kwenye mifereji,
mabonde na mito na kwamba wakati mvua zinanyesha maji hushindwa kupita kutokana
na njia za kupitisha maji hayo kuziba.
“
Wote tunatambua mafuriko yanasababishwa na nchi zilizoendelea kuchafua
mazingira kina cha Bahari ya Hindi kinazidi kuongezeka ndio maana utaona
tumejenga kuta maeneo ya mwambao wa bahari kukabiiliana na hali hii,” amesema.
Amebainisha
kuwa mafuriko yanapotokea huathiri miundo mbinu mbalimbali ikiwemo ya barabara,
madaraja na majengo kuzolewa na maji na kuongeza oparesheni hiyo itaendana na
uzibuaji wa takataka zilizoziba kwenye mitaro, mifereji na kingo za mito.
Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais,
Muungano na Mazingira Kangi Lugola akisafisha eneo la Mto Ng’ombe kuashiria
uzinduzi wa operesheni maalum ya miezi miwili ya kusafisha mito nchi nzima
Amesisitiza
kuwa wananchi wamekuwa wakitimiza wa wajibu wa kukusanya taka kwa ajili ya
kubebwa na magari ya taka ya manispaa ila watendaji wa manispaa wanashindwa
kuwajibika kusababisha wananchi kuchukua uamuzi wa kuzitupa taka hizo kwenye
maeneo yasiyotakiwa.
Amewaagiza
viongozi wote wa halmashauri za majiji, manispaa na wilaya kushiriki kikamilifu
oparesheni hiyo kwa kuhakikisha maeneo yote hatarishi yanazibuliwa kwa kugawa
vitendea kazi vya kutosha kupunguza mafuriko.
Amefafanua
kuwa baada ya miezi miwili ukaguzi utafanyika katika maeneo yote kuona kwa
kiasi gani oparesheni imefanyika na kwamba
Wakurugenzi watakaoshindwa kutekeleza agizo hilo watawajibishwa.
Aidha,
amesema Serikali ya Awamu ya Tano inawajali na kuwatahamini wananchi wake hivyo
haitakubali kuona afya za wananchi zinaathiririka kutokana na magonjwa ya
milipuko yakiwemo ya homa ya matumbo, kuhara na Kipindupindu.
Mkurugenzi
wa Manispaa ya Kinondoni, Dkt. Aaron Kagumrujuli amesema Serikali za mitaa
zinashindwa kuwasimamia wakandarasi waliopewa jukumu la kubeba taka kwenye
mitaa husika kiasi cha kuchangia uchafuzi huo.
Kwa
upande wake, Mwenyekiti wa Mtaa wa Muhalitani, Sudi Makamba amesema wananchi
wanakusanya takataka za kuziwekwa sehemu husika ila taka hizo zimekuwa zikikaa
muda mrefu bila kuzolewa na magari ya taka.
Naye
Mwenyekiti wa Mtaa wa Ali Maua, Juma Ulole Ulole amesema takataka zinazoleta
madhara eneo hilo zinatoka mbali na kuiomba Serikali kuwaletea magari ya taka
kupunguza mrundikano.
Amesema
suluhisho la mafuriko katika eneo hilo ni kuuchimba na kupanua mto unaopita
eneo hilo.
No comments:
Post a Comment