CHADEMA: Serikali inawajua waliompiga risasi Tundu Lissu..Matibabu yake zaidi ya milioni 400..soma habari kamili na Matukio360...#share

Abraham Ntambara
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo(CHADEMA) kimesema Serikali inawajua watu waliompiga risasi mbunge Tundu Lissu mkoani Dodoma.

Mwenyekiti taifa wa CHADEMA, Freeman Mbowe akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam
Pia kimesema hali ya Lissu imeimarika na mpira wa hewa, chakula na yote aliyokuwa amewekea imeondolewa na kwamba ameanza kutembea.

Kauli hiyo imesemwa na mwenyekiti taifa wa CHADEMA Freeman Mbowe jijini Dar es Salaam katika mkutano wake na waandishi wa habari.

“Serikali inawajua wote waliohusika na tukio la kumpiga risasi Tundu Lissu.” Amesema Mbowe

Ametaja baadhi ya ushahidi kuwa mara baada ya Lissu kupigwa risasi kamera zote za CCTV zilizokuwapo eneo la tukio ziliondolewa na hadi sasa hazijulikani mahala zilipo.

“Pia lile eneo alilopigwa risasi Lissu ni eneo la viongozi lina ulinzi lakini watuhumiwa wote baada ya tukio waliweza kuondoka bila kukamtwa.” Amesema Mbowe
Kuhusu hali ya afya ya Lissu, Mbowe amesema imeimarika na ametolewa mipira yote aliyokuwa amewekewa na kwamba ameanza kutembea  hadi kutoka nje.

Mwenyekiti huyo amesema pamoja na mambo mengine Lissu atapelekwa sehemu nyingine kwa   matibabu zaidi.

“Kutokana na sababu za kiusalama hatuwezi  kuweka hadharani lakini Lissu atakwenda kutibiwa mahala pengine ili kuhakikisha afya yake inatengemaa zaidi.” Amesema Mbowe.

Kuhusu gharama za matibabu, amesema yamegharimu zaidi ya milioni 400.

Pamoja na mambo mengine Mbowe amesema kuhusu taratibu nyingine za kufanya wameiachia familia ya Lissu.

“Sisi tumefanya kwa nafasi yetu lakini pamoja na mambo mengine taratibu nyingine za kufanya tumeiachia familia ya Tundu Lissu.” Amesema Mbowe


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search