Dk Tulia akabidhi milioni 40....soma habari kamili na Matukio360...#share

Naibu Spika wa Bunge  Dk Tulia Ackson amekabidhi  hundi  ya milioni 40 zitakazotumika  kwenye  ukarabati wa chumba cha upasuaji na wodi ya akinamama na watoto katika kituo cha afya cha Ruanda   Jijini Mbeya.

 Naibu Spika wa Bunge, Dk Tulia Akson akikabidhi hundi ya milioni 40.
Amekabidhi hundi hiyo leo Mkuu wa mkoa wa  Mbeya Amos Makalla na  kwamba  ni sehemu ya utekelezaji wa ahadi  aliyoitoa mwezi Machi mwaka huu.

Amesema changamoto hiyo iliwalazimisha wauguzi  kutumia rasiliamli fedha kuhamisha wagonjwa kwenda katika Hospitali ya Wazazi Meta.

“Sitoishia hapa nitakakikisha natatua kero zinazogusa kitengo cha uzazi lengo ni kuokoa maisha ya mama na mtoto wakati wa kujifungu."amesema.

Naye Amos Makalla, amemwagiza mkandarasi anayekarabati  jengo la chumba cha upasuaji na wodi ya akinamama na watoto kufanya kazi kwa weledi na kujiepusha na matumizi mabaya ya fedha hizo


Mkandarasi wa   Kampuni ya Emilet, Gilbat Mwandindile, amesema changamoto wanayokabiliana nayo ni jingo kujengwa kwa tofari mbichi.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search