Dk Tulia: Halmashauri wapimeni afya wananchi...soma habari kamili na Matukio360..#share


NAIBU Spika, Dk Tulia Ackson amezitaka halmashauri zote nchini kuendesha kampeni ya upimaji afya bure kwa wananchi ili Watanzania wawe na afya njema katika kuelekea uchumi wa viwanda.

 Wananchi waliojitokeza kupima afya bure wakimsikiliza Nibu spika  wa Bunge Dk  Tulia Ackson (hayupo pichani ) leo wakati akifunga zoezi hilo katika Viwanja vya Ruanda Nzovwe jijini mbeya..

Ametoa wito huo leo mkoani Mbeya alipokuwa akifunga kampeni ya upimaji afya bure ambapo
takribani wananchi 13,000 mkoani humo wamejitokeza kupima afya bure iliyozinduliwa  Oktoba 14 mwaka huu.

Mganga Mkuu wa Hospitali ya Mkoa huo, Seif Mhina  amesema wamevuka lengo. Walitarajia kupima wananchi 10,000. Kwa siku wananchi 2,000.

Mhina amesema idadi hiyo imeonyesha jinsi wananchi walivyohamasika na Oktoba 21,2017 wataendelea na kampeni hiyo inayoratibiwa na mkuu wa mkoa wa Mbeya, Amos Makalla. Itafanyia katika Chuo Cha Uhasibu (TIA).

Kampeni hiyo imefanywa na wataalam 86 kutoka hospitali ya Mkoa,  Rufaa ya Kanda, Jeshi, na halmashauri saba za mkoani Mbeya .

Pamoja na magonjwa mengine jumla ya wanaume 195 wamejitokeza kupima ugonjwa wa tezi dume, 26 wamekutwa na tatizo hilo na kupatiwa matibabu.

Ameitaka jamii kuwa na mwamko wa kupima afya ili kujikinga na magonjwa nyemelezi ambayo ni changamoto inayopoteza  nguvu kazi kwa taifa hususan kwa vijana.




About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search