‘Harbinder Sethi mhhhh, Mahakama yasubiri ripoti ya Muhimbili’..Soa habari kamili na Matukio360..#share

Na Salha Mohamed

MSHTAKIWA  katika  kesi ya uhujumu uchumi, Harbinder Sethi amepelekwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa ajili ya kufanyiwa vipimo.
 
Harbinder Sethi (Kulia) na James Rugemalira (kushoto)

Leo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu mwendesha mashtaka mwandamizi  wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Leonard Swai  amesema kinachosubiriwa ni ripoti ya daktari na kwamba  wiki ijayo Sethi atarudishwa  Muhimbili  kuchukua majibu ya vipimo vyake.

Wakati huo huo  wakili wa mshtakiwa James Rugemalira, Respicius Didas ameieleza mahakama hiyo kuwa kuna suala la ucheleweshwaji wa upelelezi na kwamba washtakiwa hao walifikishwa mahakamani hapo Juni 19,mwaka 2017 na wapo ndani hadi sasa.

Amelalamika kuwa  kila kesi ikifika mahakamani hapo upande wa mashtaka unadai upelelezi bado haujakamilika,  huku wateja wao wakiendelea  kukaa ndani na wanapata athari.

Akijibu hoja  Mwendesha Mashtaka  Mwandamizi wa Takukuru, Swai amedai uchunguzi wa kesi ya kughushi unachukua muda hivyo aliomba  mawakili wa upande wa utetezi wajue upelelezi bado unaendelea sheria ipo wazi katika masuala ya kughushi.

Katika kesi hiyo, washtakiwa Harbinder  Singh Sethi na James Burchard  Rugemarila wanakabiliwa na  mashtaka 12 ya  uhujumu uchumi kwa  Kula njama, kujihusisha mtandao wa uhalifu , kighushi, kutoa nyaraka za kughushi na  kujipatia fedha kwa njia za udanganyifu.

 Pia wanakabiliwa na mashtaka matano ya  kutakatisha fedha pamoja na  kusababisha hasara ya USD 22, 198,544.60 na Sh 309,461,300,158.27.

Rugemarila ni  Mkurugenzi wa VIP na mmiliki mwenza wa zamani wa IPTL na Sethi ni Mwenyekiti Mtendaji wa PAP ambapo  wanadaiwa kutenda makosa hayo kati ya oktoba 18 ,2011 na Machi 19 , 2014.

Kesi hiyo imeahirishwa hadi Oktoba 27,2017

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search