Stand United hatushuki daraja... Habari kamili soma matukio360 #share

BEKI wa kulia wa Stand United Aroun  Michael (Mokoena) amewashusha presha mashabiki wa chama hilo lenye maskani yake mjini Shinyanga kuhusu kushuka daraja msimu ujao.

Image result for timu ya soka ya Stand united
Baadhi ya wachezaji wa timu ya soka ya  Stand United wakishngalia ushindi

Stand United msimu huu wa Ligi kuu imeanza vibaya kwani mpaka sasa imecheza mechi tano na kufanikiwa kushinda moja huku nne ikipoteza.
Jambo hilo limefanya mashabiki kupata wasiwasi kwa timu yao kuwa inaweza kushuka daraja msimu ujao kutokana na matokeo hayo.
“Mashabiki wasife moyo ligi bado mbichi kabisa na kamwe hatuwezi kushuka daraja msimu ujao”alisema Mokoena.
Hata hivyo beki huyo aliwataka wachezaji wenzake kupambana kwani wanatakiwa kuanza kupata matokeo mazuri kwenye mchezo ujao na Prison mjini Mbeya.
Stand ipo nafasi ya 15 kwenye msimamo wa ligi ikiwa na alama tatu ambapo jumamosi  ya wiki hii itawavaa Prison katika mchezo utakaopigwa mkoani Mbeya.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search