UKAWA waanza tambo uchaguzi mdogo wa udiwani...Soma habari kamili na Matukio360..#share

Na Abraham Ntambara

VYAMA  vya siasa nchini vilivyounda umoja ( Chini ya mwamvuli wa UKAWA) vipo katika hatua ya mwisho wa uratibu wa jinsi vitakavyogawana  Kata 43 katika uchaguzi mdogo wa marudio wa udiwani,  utakaofanyika  Novemba 26, 2017.   
Image result for Naibu mkurugenzi wa wa Habari, Uenezi na Mahusiano na Umma-CUF Taifa, Mbarala Maharagande.
Naibu mkurugenzi wa wa Habari, Uenezi na Mahusiano na Umma-CUF Taifa, Mbarala Maharagande.
Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imesema kuwa uchaguzi mdogo wa madiwani katika kata 43 kuwa utafanyika Novemba 26 mwaka huu. Mwenyekiti wa NEC Jaji Semistocles Kaijage, amesema kuwa uchaguzi huo unafanyika kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo baadhi ya madiwani kufariki dunia, kujiuzulu, kutohudhuria vikao na wengine ushindi wao kutenguliwa na Mahakama.  
Akizungumza na Matukio360 leo jijini Dar es Salaam Naibu mkurugenzi wa wa Habari, Uenezi na Mahusiano na Umma-CUF Taifa, Mbarala Maharagande amesema uratibu wa ndani wa vyama (Kiutawala) unaendelea na maamuzi yatazingatia Utafiti wa Kisayansi unaoendelea kufanyika.
Awali tulieleza kuwa tungeweza kutoa msimamo wa mgawanyo wa Kata hizo  Oktoba 11, 2017 lakini
Oktoba 23, 2017 imepangwa kufanyika kikao cha mrejesho wa hatua mbalimbali zilizofikiwa.
Amesema  viongozi wa ngazi ya taifa watatoa tamko la pamoja kwa wakati muafaka kuonyesha mgombea wa chama kipi anapaswa kuungwa mkono katika kata husika. 
Maharagande amesema hawatarajii viongozi wa Mikoa, Wilaya na Kata kwenda kinyume na maagizo ya ngazi za Taifa na wala hakutakuwa na visingizio vya aina yeyote ile vitakavyoleta MKANGANYIKO.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search