Kesi Malkia Pembe za Ndovu kusikilizwa mfululizo...soma habari kamili na Matukio360...#share

KESI ya uhujumu uchumi ya meno ya tembo inayowakabili Salvius Matembo, Philemon Manase na raia wa China anayedaiwa kuwa Malkia wa Pembe za Ndovu, Yang Feng Glan (66)  ya bilioni 13 kusikilizwa mfululizo kuanzia Oktoba 18,19 na 20,2017.

Meno ya Tembo
Wakili wa Serikali, Paul Kadushi leo alimueleza Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Huruma Shaidi kuwa  kesi ilipaswa kuendelea kusikilizwa Oktoba 17, 2017 na kwamba walimwita shahidi mmoja  wa upande wa mashtaka lakini amepata udhuru.

Hivyo ameomba iendelee kusikilizwa Oktoba 18,2017.  Wakili wa utetezi, Nehemiah  Nkoko  alieleza kuwa alitegemea upande wa Mashtaka ungeandaa mashahidi wawili ama watatu, ili mmoja akipata udhuru wengine waendelee.

Hivyo  Hakimu Shaidi amewaambia upande wa Mashtaka wazingatie hilo na kuiahirisha hadi  kesho itakapoendelea  kwa ajili ya usikilizwaji wa ushahidi wa upande wa Mashtaka.

Washtakiwa wote walikuwepo mahakamani pamoja na Mawakili wao wanaowatetea akiwamo Nehemia Nkoko, Hassan Kihangio, Jeremiah Mtobesya.

Washtakiwa hao, wanadaiwa kuwa  kati ya Januari Mosi, 2000 na Mei 22,2014  walijihusisha na biashara  ya nyara za serikali.

Katika kipindi hicho washtakiwa hao wanadaiwa kufanya biashara ya vipande 706 vya meno ya Tembo vyenye uzito wa kilogramu 1889 zenye thamani ya Sh 5.4 bilioni  bila ya kuwa na leseni iliyotolewa na Mkurugenzi wa Wanyama Pori.

Wanadaiwa kuwa kati ya Januari Mosi, 2000 na Mei 22,2014  kwa makusudi raia wa China, China, Yang Feng Glan  aliongoza na kufadhiri vitendo vya kijinai kwa kukusanya na kusafirisha vipande hivyo 706 vya Meno ya Tembo bila ya kuwa na kibali chochote kile kutoka kwa Mkurugenzi wa Wanyama Pori.

Kwa upande wa washtakiwa Salvius na Manase wanadaiwa kuongoza makosa ya uhujumu uchumi kwa kusaidia biashara ya nyara za serikali kwa kukusanya, Kusafirisha na Kuuza Meno ya Tembo kwa nia ya kujipatia faida.

Ilidai kuwa Mei 21, 2014 katika eneo la Sinza Palestina wilaya ya Kinondoni mshtakiwa Manase alitoroka chini ya ulinzi halali wa askari wa Jeshi la Polisi D 7847 Koplo Beatus ambaye alikuwa akimshikilia kwa makosa ya kujihusisha na biashara za nyara za serikali.





About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search