TAKUKURU yamvaa Mbunge Nassari...soma habari kamili na Matukio360...#share

Salha Mohamed
TAASISI ya Kudhibiti na Kupambana na Rushwa(Takukuru) imemuonya Mbunge wa Arumeru Mashariki Joshua Nassari  kwamba aache kuishinikiza kufanya kazi na kwamba itamchukulia hatua za kisheria.

Mbunge wa Arumeru Mashariki, Joshua Nassari
Hatua hiyo inakuja kufuatia hivi karibuni  Joshua Nassari  kuikabidhi  TAKUKURU  ushahidi wake kwenye flash na harddisk pamoja na nyaraka kadhaa kwa ajili ya ushahidi wa madiwani wa Arusha kununuliwa na CCM.

Leo jijini Dar es Salaam Mkurugenzi mkuu wa Takukuru Valentino Mlowola amesema Nassari anapaswa kuzingatia sheria bila kuathiri taarifa zake alizotoa.

“Endapo Mbunge Nassari akiendelea na mwenendo huu hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yake. Pia asiingize mambo haya kisiasa.” amesema Mlowola

Mlowola amesema kwa mujibu wa sheria, inaitaka Takukuru imlinde mtoa taarifa lakini Nassari amejitangaza hadharani kupitia vyombo vya
habari.

“Mbunge Nassari anaendesha jambo hili kisiasa na si kisheria na kwa kuwa ameshaleta taarifa zake, atuache tufanye kazi yetu.” amesema










About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search