Kesi mke bilionea Msuya kuunguruma Novemba..soma habari kamili na Matukio360..#share

Na mwandishi wetu
KESI ya mauaji inayomkabili mke wa marehemu bilionea Erasto Msuya, Miriam Mrita na mfanyabiashara Revocatus Muyella itatajwa Novemba 13, 2017 baada ya jarada la kesi kufikishwa kwa Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai nchini (DCI).

Mke wa marehemu bilionea Erasto Msuya, Miriam Mrita wa pili kutoka kulia akiwa Mahakamani
Wakili wa Serikali, Patrick Mwita amedai mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba kuwa jalada  halisi la kesi hiyo limetoka ofisi ya upelelezi mkoa wa Temeke (RCO) na sasa lipo kwa DCI.

Kufuatia maelezo hayo, Hakimu Simba amepanga  kesi hiyo kutajwa  Novemba 13,2017 na amewasisitiza upande wa Mashtaka kumaliza ushahidi wao mapema

Katika kesi hiyo namba 5 ya mwaka 2017, washtakiwa hao  wanadaiwa kumuua kwa makusudi dada  wa marehemu bilionea, Erasto Msuya, Aneth Msuya.

Tukio hilo, linadaiwa kufanywa Mei 25, 2016 maeneo ya Kibada Kigamboni Jijini Dar es Salaam.

Washtakiwa hao, awali  Februari 23, 2016, waliachiwa huru katika kesi ya mauaji namba 32 ya mwaka 2016 na Hakimu Mkazi Mwandamizi Godfrey Mwambapa.


Baada ya kufutwa kwa kesi hiyo iliyokuwa ikifanana na hii walikamatwa  na baadaye kusomewa mashtaka hayo ya mauaji upya.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search