Shahidi kesi Malkia pemba za ndovu augua...soma habari kamili na Matukio360..#share
Na
mwandishi wetu
SHAHIDI upande wa mashtaka aliyetarajiwa kutoka ushahidi katika kesi inayomkabili raia wa China, Yang Feng Glan (66) ‘Malkia wa Pembe za Ndovu’ na wenzake wawili, anaumwa.
Baadhi ya pembe za ndovu
Hayo
yameelezwa leo na wakili wa serikali, Simon Wankyo mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakam aya Kisutu,
Huruma Shaidi.
Wankyo
amedai kesi hiyo ilipangwa kwa ajili ya
kuendelea kusikilizwa kwa ushahidi wa mashahidi wa upande wa mashtaka na kwamba
ushahidi waliyemtarajia atoe ushahidi anaumwa na hali yake bado siyo nzuri.
Hivyo
ameomba ipangiwe tarehe nyingine kwa ajili ya kuendelea kusikilizwa na wakili wa
utetezi, Nehemia Nkoko hakuwa na pingamizi.
Hakimu
Shaidi ameahirisha hadi Novemba 7,2017 na kuamuru siku hiyo upande wa mashtaka
upeleke mashahidi.
Washtakiwa
wengine wanaokabiliwa na kesi hiyo ni Salvius Matembo na Philemon Manase ambao
kwa pamoja, wanadaiwa kuwa kati ya
Januari Mosi, 2000 na Mei 22,2014
walijihusisha na biashara ya
nyara za serikali.
Katika
kipindi hicho washtakiwa hao wanadaiwa kufanya biashara ya vipande 706 vya meno
ya Tembo vyenye uzito wa kilogramu 1889 zenye thamani ya Sh 13 bilioni bila ya kuwa na leseni iliyotolewa na
Mkurugenzi wa Wanyama Pori.
Wanadaiwa
kuwa kati ya Januari Mosi, 2000 na Mei 22,2014
kwa makusudi raia wa China, China, Yang Feng Glan aliongoza na kufadhiri vitendo vya kijinai
kwa kukusanya na kusafirisha vipande hivyo 706 vya Meno ya Tembo bila ya kuwa
na kibali chochote kile kutoka kwa Mkurugenzi wa Wanyama Pori.
Kwa
upande wa washtakiwa Salvius na Manase wanadaiwa kuongoza makosa ya uhujumu
uchumi kwa kusaidia biashara ya nyara za serikali kwa kukusanya, Kusafirisha na
Kuuza Meno ya Tembo kwa nia ya kujipatia faida.
Ilidai
kuwa Mei 21, 2014 katika eneo la Sinza Palestina wilaya ya Kinondoni mshtakiwa
Manase alitoroka chini ya ulinzi halali wa askari wa Jeshi la Polisi D 7847
Koplo Beatus ambaye alikuwa akimshikilia kwa makosa ya kujihusisha na biashara
za nyara za serikali.
No comments:
Post a Comment