MAGUFULI: Mimi ni kibarua, Meli mpya kutengenezwa...soma habari kamili na Matukio360..#share

Na Mwandishi wetu
 RAIS Dk John Magufuli amesema yeye ni kibarua wa Watanzania na kwamba pamoja na changamoto zote atawatumika kwa moyo wa uadilifu na uaminifu.



Rais wa Tanzania, Dk John Pombe Magufuli
Pia amesema Serikali itatengeneza Meli mpya yenye uwezo wa kubeba abiria 1200 na kupanua uwanja wa ndege jijini Mwanza.

Ametoa kauli hiyo Leo jijini Mwanza alipokuwa akifungua rasmi matumizi ya daraja jipya la waenda kwa miguu la Furahisha. Linauwezo wa kupitisha watu 60 kwa wakati mmoja

“Mimi ni kibarua wenu, nitakutumikieni kwa moyo mmoja. Naamini kila kitu kipya ni miujiza na haya ninayofanya na kuahidi ni kama miujiza lakini namuomba Mungu iwe kweli, ” amesema rais Magufuli

Amesema daraja hilo lililochorwa na waadisi na kujengwa na wakandarasi  wazalendo halipo mahala popote nchini.

‘Jamani haya ndio maendeleo pamoja na mambo mengine limejengwa na wazalendo na halipo mahala popote nchini. Linajiwasha taa lenyewe,’ amesema

Rais amesema mkakati wa serikali ni kuufanya mkoa wa Mwanza kuwa kiunganishi katika biashara na kwamba itatengeza meli mpya.

Amesema kampuni moja kutoka Korea Kusini imeshinda tenda ya utengenezaji wa meli hiyo itakayokuwa na uwezo wa kubeba abiria zaidi 1200, tani za kutosha za mizigo na magari.

‘Tayari hawa  watu wa Korea Kusini wameshafika hapa Mwanza tangu jana jioni na leo wataanza kukagua mahala pazuri pa kujengea hiyo meli, wakikamilisha hayo tutasaini mkataba na mwisho wa mwezi wa kwanza, 2018 ujenzi utaanza,’ amesema rais  

Mbali na meli hiyo, rais Magufuli amesema serikali itazifanyia ukarabati meli ya Mv Victoria na Liemba ya mkoani Kigoma ziweze kuwa katika ubora.

Amesema fedha zote zinatolewa na serikali na kwamba upanuzi wa uwanja wa ndege wa Mwanza utaanza mara tu baada ya mazungumzo kati ya serikali, wahisani na wafadhili kukamilika. Amesema lengo ni uwanja wa ndege wa Mwanza kuwa wa kimataifa.

Rais ameongeza kuwa ujenzi wa  barabara  mpya inayowekwa lami ya kutoka Kisesa kwenda Usegera umekamilika kwa asilimia 80 lengo ni kupanua uchumi wa Mwanza.

Amesema upembuzi yakinifu unafanyika wa ujenzi wa barabara wa kilomita tatu za lami kutoka Busisi hadi Kigongo. ‘Pia tunazifanyia uboreshaji na upanuzi hospitali za Mwanza ikiwamo ya seketule,’ amesema 

Pamoja na mambo mengine amesimamisha bomoabomoa  za nyumba katika baadhi ya maeneo jijini humo.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search