Kesi mke bilionea Msuya yanguruma... RTO Temeke atakiwa kufika Mahakamani...soma habari kamili na Matukio360...#share


 KESI ya mauaji inayomkabili mke wa marehemu bilionea Erasto Msuya, Miriam Mrita na mfanyabiashara Revocatus Muyella imeendelea leo huku Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ikiamuru mkuu wa  upelelezi wa makosa ya Jinai  wa Temeke (RCO) afike mahakamani hapo kueleza upelelezi umefikia wapi.



Mke wa marehemu bilionea Msuya,Miriam Mrita akiwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu

Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba ametoa agizo hilo leo  wakati kesi hiyo ilipotajwa na kusisitiza  ni lazima afike mwenyewe Oktoba 30,2017  bila ya kutoa udhuru.

Uamuzi huo umefuatia baada ya wakili wa Serikali, Patrick Mwita kuieleza mahakama kuwa upelelezi wa kesi hiyo upo katika hatua za mwisho kukamilika na jalada lipelekwe kwa Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP).

Katika kesi hiyo namba 5 ya mwaka 2017, washtakiwa hao  wanadaiwa kumuua kwa makusudi Dada  wa marehemu bilionea, Erasto Msuya, Aneth Msuya.

Tukio hilo, linadaiwa kufanyika Mei 25, 2016 maeneo ya Kibada Kigamboni Jijini Dar es Salaam.

Februari 23, 2016 washitakiwa hao  waliachiwa huru katika kesi ya mauaji namba 32 ya mwaka 2016 na Hakimu Mkazi Mwandamizi Godfrey Mwambapa.

Baada ya kufutwa kwa kesi hiyo iliyokuwa ikifanana na hii walikamatwa  na baadaye kusomewa mashtaka hayo ya mauaji upya.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search