Wapiga debe kuvaa sare...soma habari kamili na Matukio360...#share

SERIKALI Mkoani Mbeya imewaagiza wapiga debe katika kituo kikuu cha mabasi ya mikoani kuwa na sare  zitakazowatambulisha ili kukabiliana na matukio ya uharifu ikiwamo ukabaji, uporaji na utapeli.



Mkuu wa mkoa wa Mbeya Amos Makalla


Mkuu wa mkoa  huo Amos Makalla, ameimbia Matukio360 kuwa ni wakati muafaka kwa wapiga debe kituoni hapo kuwa na sare za utambulisho wao. Kituo hicho kimegharimu zaidi ya milioni 35.

Amesema utaratibu huo ukifuatwa  utapunguza kwa kiasi kikubwa matukio mbalimbali ya kiharifu.

na kwamba wapigadebe hao  wawafichue waharifu.

"Wapiga debe wengi  ni waharifu na wanatambuna tabia hizo sasa nawaagiza wachague uongozi, wawe na sare zitakazowatambulisha kisheria,” amesema

Pia amewataka  wafanyabishara kituoni hapo kuzingatia kanuni za usafi ili kujikinga na  maradhi mbalimbali ikiwamo  ugonjwa wa kipindupindu.

Naye diwani  wa kata ya Sisimba Geofrey Kajigili (Chadema) ameiomba Serikali kukarabati kituo cha polisi na ujenzi wa choo  kufuatia kuchakaa.

Amesema kituo cha polisi hakina mazingira mazuri kiusalama na kwamba  Serikali iweke mikakati ya  kukiboresha.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search