Kesi mtandaoni ya ACACIA yanguruma...soma habari kamili na Matukio360...#share

UPELELEZI wa kesi ya kusambaza taarifa za uongo kupitia mtandao wa kijamii  wa Face book kuhusu mazungumzo kati ya Serikali na wawakilishi wa kampuni ya Acacia, inayomkabili mkazi wa Chato Geita, Obadia Kiko (41), katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu  haujakamilika.
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu
Hayo yameelezwa jana na Wakili wa Serikali, Adolf Mkini kwa Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri wakati kesi hiyo ilipotajwa.

Baada ya kutolewa kwa maelezo hayo, Hakimu Mashauri aliiahirisha kesi hiyo hadi Novemba 14,2017 kwa ajili ya kutajwa.
Katika kesi hiyo, mshtakiwa  anadaiwa  Agosti 3,2017 huko Chato Geita alifanya kosa hilo kupitia mtandao wa Face book.

Mshtakiwa anadaiwa kusambaza maneno kuwa " Taarifa kutoka kikao cha mazungumzo kati ya Serikali na wawakilishi wa kampuni ya Acacia kuwa wanasheria wa upande wetu wanashindwa kutafsiri baadhi ya vifungu vya sheria hadi kufikia kuomba msaada kwa wanasheria wa Acacia sasa huoni hivi ni vituko mwizi anakusaidia sheria haahaa haha."

Inadaiwa aliendelea kusambaza maneno kuwa "Mazungumzo bado yanaendelea lakini wanasheria wetu wamebanwa sana ukizingatia wale jamaa wana vielelezo vyote vya mikataba kiukweli tumuombe mungu maana Serikali ikitaka kuvunja mkataba na Acacia gharama kubwa zitatuhusu."

"Lakini pia kuendeleza uvyama utatugharimu saana,  baada ya mh. Rais Magufuli angewashirikisha Mawakili wasomi waliokwishaiva wakili Lissu, wakili Kibatara na Fatma Karume kwenye mambo ya umuhimu kama haya yeye kaleta uchama sasa itatugharimu .// Dicteta Magufuli mist go" . Maneno hayo yanadaiwa kusambazwa na mshtakiwa huyo kupitia mtandao huo wa kijamii wa Facebook.


Imedaiwa maneno hayo yalikuwa na lengo la kupotosha umma.  Mshtakiwa amekana shitaka hilo  na yupo nje kwa dhamana.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search