Maiti zaendelea kuopolewa Somalia...soma habari kamili na matukio360...#share

MIILI ya watu waliouawa kwenye mlipuko mkubwa wa bomu katika eneo lenye shughuli nyingi kwenye mji mkuu wa Somalia Mogadishu siku ya Jumamosi, imeendelea kuopolewa huku miili 160 ikizikwa jana na serikali kutokana na kutotambulika.

Mwili ukiopolewa kutoka katika moja ya jengo lililovunjika kutokana na milipuko ya mabomu Mogadishu Somalia
Inadaiwa idadi ya waliokufa hadi sasa imefikia zaidi ya watu 300, kwa mujibu wa ripoti ya shirika la habari la Reuters na kwamba takriban watu wengine 300 wamejeruhiwa kwa mujibu wa AFP, wakati lori lililokuwa limejazwa vilipuzi lilipolipuka karibu na lango la hoteli.

Ahmed Ali ambaye ni  mwuguzi anayefanya kazi kwenye hospitali moja mbali na miili 160 iliyozikwa na serikali miili mingine ilizikwa na jamaa zao.

Hilo ndilo shambulizi baya zaidi kutokea nchini Somalia tangu kundi la al-Shabab lianzishe harakati zake mwaka 2007.
Rais Mohamed Abdullahi "Farmajo" Mohamed alilaumu kundi la al-Shabab kwa shambulizi hilo katili.
Rais huyo alichangia damu na tayari Uturuki imefungua kambi kubwa ya kijeshi Somalia


"Tumethibitisha kuwa watu 300 waliuawa kwenye mipuko huo. Idadi ya waliokufa huenda bado ikaongezeka na kuna watu kadha ambao bado hawajulikani waliko," Abdikadir Abdirahman, mkurugenzi wa idara ya magari ya kusafirisha wagonjwa aliliambia shiria la Reuters.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search