Kesi ya Mwenyekiti CCM Yapigwa na Wenzake Yapigwa Kalenda'..Soma Habari Kmili matukio360..#shar

KESI inayomkabili Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Mbunge wa Geita Joseph Msukuma na madiwani nane imesogezwa mbele baada ya upande wa mashitaka kudai upelelezi haujakamilika.
Mbunge wa Jimbo la Geita,na Mwenyekiti wa chama cha mapinduzi CCM Mkoani Geita ,Joseph Kasheku(Msukuma) akiteta jambo  nje ya mahakama baada ya kesi kuhailishwa
Kesihiyo ambayo ilikuwa isikilizwe leo imepangwa kutajwa tarehe 10 mwezi wa 11 mwaka huu ambapo washitakiwa wote wapo nje kwa dhamana.

Kwa upande wake wakili anayewatetea washitakiwa Bw Deo Mgengeli ameelezea hatua ambayo imeendelea siku ya leo mahakamani hapo kuwa shauri limekuja na kwamba limetajwa na hadi sasa hakuna mshitakiwa ambaye ameongezeka hivyo mahakama imeamua tarehe Kumi mwezi wa 11 wawasili mahakamani kusikiliza tena kesi hiyo.

Aidha wakili Mgengeli amezungumzia suala la madiwani wengine waliokamatwa na jeshi la polisi na kutofikishwa mahakamani  amesema kuwa kukamatwa  kwa madiwani hao  ni jambo la kawaida  kwani ni swala la upepelezi kwa makosa ya jinai na kwamba alhamisi wanatakiwa kwenda tena polisi ili kujua ni kipi ambacho kinaendelea ila hadi sasa awana kosa lolote.

Awali washitakiwa hao kwa pamoja walifikishwa
katika mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Geita Septemba 19 mwaka huu.

Washitakiwa wanakabiliwa mashitaka ya kufanya mkutano bila kibali, kuziba barabara na uharibifu wa bomba la maji linaloelekea kwenye mgodi wa dhahabu wa GGM.


Baadhi ya wananchi ambao walijitokeza kusikiliza kesi hiyowakiwa nje ya mahakama.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search