Simba ikivaa Yanga Aveva, Kaburu mambo bado magumu..soma habari kamili na Matukio360..#share
Na Mwandishi wetu
WAKATI
zikiwa simesalia siku chache watani wa jadi katika soka Simba na Yanga kuvaana
rais wa klabu ya Simba, Evans Aveva na Makamu wake,Godfrey Nyange ‘Kaburu’ hadi
sasa, jarada la uchunguzi la kesi inayowakabili ya utakatishaji wa fedha dola
za kimarekani 300,000 bado lipo kwa Mkurugenzi wa Mashtaka ,(DPP).
Aveva na Kaburu wakiingia katika moja ya chumba cha Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu
Wakili
wa Serikali mkuu, Vitalis Peter ameeleza hayo leo kwa Hakimu Mkazi Mwandamizi,
Victoria Nongwa na kuwa kesi hiyo ilipangwa kwa ajili ya kutajwalakini jalada
la uchunguzi bado lipo kwa DPP na ameomba kesi hiyo ipangiwe tarehe nyingine.
Hata
hivyo Wakili wa washtakiwa hao, Evodius Mtawala amedai kuwa upande wa
mashtaka Septemba 18,2017 ulitoa taarifa
kuwa jalada la uchunguzi wa kesi hiyo lipo kwa DPP.
Mtawala
amedai tangu siku hiyo ni siku 37 zimepita hivyo ameiomba Mahakama iwahimize
upande wa mashtaka kulifuatilia jalada hilo kwa DPP kwa sababu wateja wake wapo
ndani na maisha yao yamekuwa ni kama yamesimama.
Akijibu
hoja hizo za Wakili Mtawala, Mwendesha Mashtaka Mwandamizi wa Taasisi ya Kuzuia
na Kupambana na Rushwa (Takukuru),Leonard Swai amedai kuwa ni kweli na kwamba
wanajitahidi kulifuatilia lakini hadi sasa bado halijatoka kwa DPP.
Hata
hivyo, Swai amedai sheria haijampa muda
DPP wa kukaa na jalada ila kwa upande wao ni kuhimiza tu.
Hakimu
Nongwa baada ya kusikiliza hoja hizo, aliwataka upande wa Mashtaka walifuatilie
na ameiahirisha kesi hadi Novemba 6,2017.
Evans
Elieza Aveva na makamu wake, Geofrey
wanakabiliwa na mashtaka matano ya kughushi, kuwasilisha nyaraka ya uongo na
kutakatisha fedha USD 300,000.
Katika
shtaka la kwanza, washtakiwa hao wanadaiwa kuwa
walikula njama ya kughushi fomu ya maombi ya kuhamisha fedha ya Machi
15,2016 wakionesha Klabu ya Simba inalipa mkopo wa USD 300,000 kwa Evans Aveva wakati si kweli.
Katika
shtaka la pili alidai kuwa Machi 15,2016 katika benki ya CRDB tawi la Azikiwe
Ilala Aveva akijua alitoa nyaraka za uongo ambayo ni fomu ya maombi ya
kuhamisha fedha ya Machi 15,2016 wakati akijua ni kosa.
Katika
la tatu la kutakatisha fedha, Aveva na Nyange wanadaiwa kuwa kati ya Machi 15
na Juni 29,2016 Dar es Salaam kwa pamoja
walikula njama ya kutakatisha fedha kwa kupata USD 300,000 wakati wakijua ni
zao la uhalifu.
Kwa
upande wa shtaka la nne la kutakatisha fedha, Aveva anadaiwa kuwa kati ya Machi
15,2016 katika benki ya Baclays Mikocheni alijipatia USD 300,000 wakati akijua
zimetokana na kughushi.
Katika
shtaka la tano la kutakatisha fedha, mshtakiwa Nyange anadaiwa kuwa Machi 15,2016 katika benki ya Baclays tawi la
Mikocheni alimsaidia Aveva kujipatia USD
300,000 wakati akijua fedha hizo zimetokana na kughushi.
Washtakiwa
wapo rumande kwa sababu shtaka la kutakatisha fedha linalowakabili halina
dhamana.
Simba
ya Yanga zinatarajiwa kupambana Oktoba 28, 2017 katika uwanja wa Uhuru ‘shamba
la bibi’ jijini Dar es Salaam
No comments:
Post a Comment