Kesi ya vigogo wa Wizara Nishati, Madini yaunguruma..Soma habari kamili na Matukio360..#share

UPELELEZI wa kesi  inayomkabali mthamini wa madini ya Almas wa serikali, Edward Joseph Rweyemamu(50) na Mkurugenzi wa tathimini, Archard Alphonce Kalugendo(49) umekamilika kwa kiasi kikubwa.
 
Mkurugenzi wa Tathmini, Archard Alphonce Kalugendo (49) na Mthamini wa Madini ya Almas wa Serikali, Edward Joseph Rweyemamu (50) wakitoka katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.

Wakili wa Serikali, Wankyo Simon ameeleza hayo leo kwa Hakimu Mwandamizi, wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Godfrey Mwambapa wakati kesi hiyo ilipotajwa.

Wakili Wankyo amedai  upelelezi wa kesi hiyo bado unaendelea na wamewaelekeza polisi kufanya upelelezi na tayari sehemu kubwa ya upeleleze umekamilika.

Amedai kutokana na hali hiyo, tarehe ijayo wataieleza Mahakama upelelezi huo  umefikia  hatua gani.

Kufuatia  maelezo hayo, Hakimu Mwambapa ameahirisha kesi hiyo hadi Oktoba 26,2017.

Washtakiwa hao wanakabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi kwa  kusababisha hasara ya dola za Kimarekani 1,118,291.43 sawa na Sh 2,486,397,982.54.

Kalugendo ambaye ni mkazi wa Kinyerezi na Rweyemamu mkazi wa Mwananyamala wote ni waajiriwa wa wizara ya Nishati na  Madini.

Kati ya Agosti 25 na ,31, 2017 katika maeneo mbalimbali kati ya Dar es Salaam na Shinyanga, washtakiwa hao kwa pamoja na kwa vitendo vyao wakiwa wathamini walioajiliwa na Wizara ya Nishati na Madini walisababisha hasara ya kiasi hicho cha fedha.


Baada ya kusomewa shtaka hilo, washtakiwa hao hawakuruhusiwa kuongea chochote kwa sababu Mahakama ya Kisutu haina mamlaka ya kusikiliza kesi hiyo hadi Mahakama Kuu. Washtakiwa wapo rumande.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search