Masogange kuanza kujitetea kesi ya dawa za kulevya..Soma habari kamili na Matukio360..#share

MSANII maarufu wa unogeshaji wa video (Video Queen) Agnes Gerald(Masogange) ataanza kujitetea katika kesi inayomkabili ya matumizi ya dawa za kulevya Novemba 14, 2017.

Video Queen, Agnes Gerald maarufu kama Masogange akizungumza na wakili Rouben Semwanza leo mara baada ya kufika katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam .

Mshtakiwa huyo alipaswa kuanza kujitetea leo katika mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu lakini  Wakili wa Serikali, Adolf Mkini aliomba kwa Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri ipangiwe tarehe nyingine.

Kufuatia maelezo hayo, Hakimu Mashauri ameiahirisha hadi Novemba 14, 2017 ambapo ataanza kutoa utetezi wake.

Pia hatua hiyo imefikiwa baada ya Hakimu Mashauri kumuona mshtakiwa Masogange  ana kesi ya kujibu na anapaswa kujitetea na kuwaita mashahidi ambao ni  watatu.

Masogane anatetewa na Mawakili  Nehemia Nkoko na Ruben Simwanza.

Kesi hiyo inaendeshwa na  Wakili wa Serikali, Costantine Kakula na wanamashahidi watatu

Masogange anakabiliwa na mashtaka mawili ya kutumia dawa za kulevya aina ya Heroin na Oxazepam.

Anadaiwa kufanya makosa hayo chini ya kifungu cha 18 (a) cha sheria ya kupambana na dawa za kulevya namba 5 ya mwaka 2015.

Katika kesi hiyo namba 77 ya mwaka 2017, Masogange anadaiwa  kati ya Februari 7 na 14,2017 katika maeneo yasiyojulikana ndani ya jiji la Dar es Salaam  alitumia dawa za kulevya aina ya Heroin (Diacety Imophine).


Pia anadaiwa kuwa kati ya Februari 7 na 14,2017  alitumia dawa za kulevya aina ya Oxazepam.

Video QUeen, Agnes Gerald maarufu kama Masogange akitoka katika mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu mara baada ya kusomewa mastaka yanayomkabiri ya matumizi ya Dawa za kulevya na kesi yake kupigwa Kalenda mpaka Novemba 14, 2017.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search