Liverpool, Man U hakuna mbabe... habari kamili soma Matukio360..#share
TIMU
ya soka ya Liverpool na Manchester United zimetosha nguvu baada ya kwenda sare
ya bila kufungana.
Kipa wa Man U, David De Gea akiokoa mpira katika mechi na Liverpool
Mchezo
huo liochezwa katika uwanja wa Anfield kwa sehemu kubwa ulitawaliwa na
Liverpool kwa kulishambulia lango la Man
U ambao kwa muda mwingi walikuwa wakizuia.
Kufuatia
mechi hiyo Man u imefikisha pointi 20 katika mechi nane iliyocheza huku
Liverpool ikifikisha pointi 13.
Klabu
hizo mbili ni mahasimu wakuu mashabiki wa timu hizo wanauadui wa kihistoria.
Katika
mpambano huo Meneja wa Liverpool Jurgen Klopp alikuwa akiadhimisha miaka miwili
tangu atue Liverpool
Katika
mechi hiyo Liverpool ilimkosa mchezaji wake tegemeo Sadio Mane aliyeumia misuli
ya paja akichezea Senegal mechi za kufuzu Kombe la Dunia lakini Klopp anaamini
wanaweza kujimudu bila yeye.
Mane
anatarajiwa kukaa nje wiki sita.
United walimkosa kiungo wa kati Marouane Fellaini kutokana na kuumia kano za goti akichezea
Ubelgiji. Pia na nahodha Michael Carrick ambaye bado anauguza jeraha
Wachezaji
wengi wa timu mbalimbali wametoka kuchezea timu za taifa na majeraha - ni
tatizo kubwa kutokana na mabadiliko ya mtindo wa mazoezi na uchezaji pia.




No comments:
Post a Comment