Rais Magufuli ampiga kijembe Maalim Seif... Kuingiza bilioni 159 aokoa bilioni 86...soma habari kamili na Matukio360...#share




NDIVYO unavyoweza kusema hicho ni kijembe kufuatia rais wa Tanzania  Dk John Magufuli kushangazwa na kauli kuwa Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif ataapishwa kuwa rais wa Zanzibar.


Rais Dk John Magufuli akimsikiliza kwa makini rais mstaafu wa awamu ya pili Alhaji Hassani Mwinyi

“Hivi karibuni wapo wengine wamejitapa wataapishwa eti kuwa rais wa Zanzibar lakini mbona hadi sasa ajaapishwa.”



Rais Magufuli amesema hayo leo mjini Zanzibar alipokuwa akihutubia katika maadhimisho ya kumbukizi ya miaka 18 ya kifo cha rais wa kwanza wa Tanzania, Mwalimu Julias Nyerere, kilele cha mbio za mwenge na siku ya vijana kitaifa



Pia amesema katika mwezi ujao serikali  itaingiza zaidi ya bilioni 159 kwa ajili ya mishahara na malupulupu kwa wafanyakazi wa serikali na kwamba imeokoa zaidi ya bilioni 86 ambazo zingelipwa kwa wafanyakazi hewa.



Amesema si kwamba  hataki kuongeza mishahara na kwamba hilo linategemeana na hali halisi ya mahitaji ya nchi kwa wakati husika.

“Si kwamba sitaki kuongeza mishahara na malupulupu ila ni vigumu kutekeleza hilo wakati nchi inahitaji kufanya mambo mengi ya kusaidia watanzania. Pia upo uwezekano huo,” amesema na kuongeza



“Mwezi ujao serikali itaingiza zaidi ya bilioni 159 katika mishahara na imeokoa zaidi bilioni 86 ambazo zingelipwa kwa wafanyakazi hewa.”



Hata hivyo, Rais Magufuli amesema halizishwi na mashinikizo yanayotolewa na wadau mbalimbali kuhusu ongezeko la mishahara na malupulupu.



“Kusiwepo na shinikizo la kulazimisha kudai ongezeko la mishahara na malupulupu.” amesema


Rais anatoa msimamo huo ikiwa ni siku moja baada ya msemaji mkuu wa serikali na mkurugenzi wa habari maelezo Dk Hassan Abas kukanusha taarifa kuwa rais Magufuli hataki kupandisha mishahara na kwamba  chama cha wafanyakazi nchini (Tucta) kisitumike kisiasa kwa kudai kusikitishwa na kutopandashwa mishahara.



Hivi karibuni kumekuwapo na taarifa inayomuhisisha katibu mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad kuwa anadai ataapishwa kuwa rais wa Zanzibar.

  


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search