Lowasa ampokea Nyalandu CHADEMA, LHRC wampongeza...soma habari kamili na Matukio360..#share

Na Abraham Ntambara

MJUMBE wa kamati kuu ya Chadema, Edward Lowassa amemkaribisha Lazaro Nyalandu katika chama hicho huku kituo cha Sheria na Haki za Binadamu  (LHRC) kikiunga mkono hoja za kujivua Ubunge na kuachia nyazifa zote ndani ya Chama cha Mapinduzi (CCM)   kwa Nyalandu ambaye  aliwahi kuwa Waziri wa Maliasili na Utalii katika Serikali ya Awamu ya Nne, Lazaro Nyalandu.
Mkurugenzi wa Mtendaji wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu Dk. Hellen Kijo Bisimba.

Mapema leo Nyalandu ametangaza kuchukua hatua hiyo kwa kile anachodai kuwa hali ya sasa ya kisiasa nchini siyo nzuri kutokana na kuwepo ukandamizaji wa Demokrasia kwa kuminya uhuru wa kijeleza na kutoa maoni pamoja na matendo yanayoashiria uvunjifu wa Katiba .

Akizungumza leo na Matukio360 Mkurugenzi Mtendaji wa LHRC Dk. Hellen Kijo Bisimba, amesema kitendo cha Nyalandu kuhama CCM ni haki yake  ya Kikatiba na kueleza kuwa sababu alizotoa za kuhama ni za msingi kutokana nchi kupitia kwenye kipindi kigumu katika masula ya Demokrasia.

Aidha  amesema kwa sasa  kitendo cha Nyalandu kuibuka na kusema hadharani ni ishara ya kuchoka kukishauri chama  hicho bila kusikilizwa hivyo akaamua kujiandoa mwenyewe na kusema hadharani .

“Nyalandu anahaki kama raia ya kufanya uchambuzi  wa masuala yanayoendelea, sisi kama watetezi wa haki za binadamu tunaweza kukubaliana naye kutokana na kuwepo kwa vitendo vya ukandamizaji ikiwemo kutokuwepo na haki ya kujieleza, akiwa ndani ya CCM amefanya uchambuzi ameyaona hayafai” amesema Dk. Bisimba.

Ameongeza kuwa uongozi wa kipindi kilichopita wa Serikali ya  CCM ulikuwa ukitoa uhuru wa kujieleza na kuruhusu wananchi kuikosoa lakini kwa sasa hali imebadilika.

“Tumezoea miaka iliyopita uhuru ulikuwepo,lakini sahivi licha ya kuwepo kwa Haki za binadamu lakini kumekuwepo kwa sheria kandamizi ikiwemo sheria ya mtandao,leo uhuru wa Kikatiba wa kukusanyika umeminywa,Tunashuhudia Wabunge wakikamatwa”

“Kwa mfano tumeshuhudia mbunge wetu wa Kawe (Halima Mdee) amekamatwa kwa amri ya mkuu wa Wilaya na hata Rais anashindwa kumchukulia hatua Mkuu huyo wa Wilaya “ amesema Dkt Bisimba.

Dkt Bisimba amewataka wanajamii kutobeza uamuzi wa Nyalandu kwani ni haki yake Kikatiba.

Naye Lowassa amemkaribisha kwa mikono miwili Nyalandu na kwamba Chadema ndio mahala panapomfaa


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search