Wa-Iran kumi, Watz wawili wa dawa za Heroin wapandishwa kizimbani..soma habari kamili na Matukio360..#share

Na mwandishi wetu
Wa-Iran kumi na Watanzania wawili leo wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wakikabiliwa na mashtaka matatu ikiwamo  la  kusafirisha dawa za kulevya aina ya Heroin kilo 111.02

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu
Wakili wa Serikali Mwandamizi, Kishenyi Mutalemwa amedai mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi, Victoria Nongwa kuwa Oktoba 25, 2017 watuhumiwa hao walikutwa katika ukanda wa bahari ya Hindi upande wa Tanzania wakisafirisha kilo 111.02 za Heroin na bangi  gramu 235.78

Imedaiwa siku hiyo washtakiwa hao walichanganya dawa za kulevya aina ya Bangi na Kuberi zenye uzito wa kilo 3.34.

Baada ya kusomewa mashtaka hayo washtakiwa hao hawakuruhusiwa kuongea chochote kwa sababu mahakama hiyo haina mamlaka ya kuisikiliza kesi hiyo. Walikuwa wakitafsiriwa lugha ya kiswahili kwenda Kiirani na mkalimani Meja Ndakeye (45)
Upande wa mashtaka umedai  upelelezi bado haujakamilika na washtakiwa wamepelekwa rumande hadi Novemba 13,2017 itakapotajwa.

Hata hivyo kutokana na kiwango cha dawa  kuwa kikubwa mahakama ya Kisutu haina mamlaka kutoa   dhamana  kwa washtakiwa hao.

Washtakiwa hao ni Nabibakshsh Bibarde40, Mohammed Dorzade (23), Abdallah Sahib, Ubeidulla Abdi, Naim Ishaqa, Moslem Amiree, Rashid Badfar, Omary  Ayoub, Tahir Mubarak, Abdulmajid Asqan, Ally Abdallah na Juma Juma.



About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search