Tanzania yazidi kuporomoka Duniani...soma habari kamili na Matukio360..#share

Shirikisho la soka duniani Fifa limetoa orodha mpya ya viwango vya soka duniani baada ya kuchezwa kwa mechi za kufuzu kwa Kombe la Dunia 2018, Kenya na Tanzania zikishuka zaidi ya hatua 10 kwenye orodha hiyo..
Mchezaji wa kimataifa wa Tanzania, Mbwana Samatta
Ujerumani bado wanaongoza wakifuatwa na Brazil na Ureno.
Tanzania inashikilia nafasi ya 136 sasa baada ya kushuka nafasi 11, Kenya nayo imeshuka nafasi 14 hadi nafasi 102.

Katika mechi za kirafiki ambazo Harambee Stars walicheza hivi majuzi, walilazwa 1-0 na Thailand baada ya kuchapwa 2-1 na Iraq mjini Basra.

Burundi imesalia nafasi ya 129, Uganda ikapanda hatua moja hadi nafasi ya 70.
Malawi imeshuka nafasi moja hadi nambari 117 ambapo inafuatwa katika nafasi ya 118 na Rwanda ambao bado walishikilia nafasi hiyo katika orodha iliyotangazwa awali.

DR Congo wamepanda nafasi 7 hadi nafasi ya 35.
Afrika Tunisia wanaongoza kiwa nafasi ya 28 duniani baada ya kupanda hatua 3 wakifuatwa na Misri walio nafasi ya 30 duniani
Orodha ya Fifa
Nafasi Taifa
1          Ujerumani
2          Brazil
3          Ureno
4          Argentina
5          Ubelgiji
6          Poland
7          Ufaransa
8          Uhispania
9          Chile
10        Peru
11        Uswizi
12        England
13        Colombia
14        Wales
15        Italia
16        Mexico
17        Uruguay
18        Croatia
19        Denmark

20        Uholanzi

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search