Mbeya kutoa asilimia 10 ya mapato kwa wanawake na vijana..Soma habari kamili na Matukio360..#share


MKUU wa Mkoa wa Mbeya Amos Makalla, ameagiza halmashauri zote kutoa asilimia 10 ya mapato ya ndani kwa vikundi vya  wanawake na vijana ili kutekeleza lengo la serikali kuwezesha makundi hayo
Image result for AMOS MAKALA
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Amos Makalla

Akizungumza na Matukio360 Makalla amesema ameziagiza  halmashauri kutoa fedha hizo.

"Tayari nimeagiza halmashauri zote kuhahakisha fedha  zinatolewa kwa wakati na si kwa kificho na kwamba  vyombo vya habari  vishirikishwe,"amesema

Aidha amesema katika  halmashauri saba za mkoani Mbeya, halmashauri ya chunya inaongoza kimkoa na kitaifa kwa utoaji wa mikopo kwa wanawake na vijana huku jiji la mbeya likishika mkia

Awali mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya Chunya Sophia Kumbuli amesema  mwaka 2016/17  imetolewa mikopo ya zaidi milioni 300  kwa wanawake na vijana katika mapato yake ya ndani


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search