Miili ya waliouawa DRC yapatikana...soma habari kamili na Matukio360...#share

Jeshi la Jamuhuri ya Kidemokrasi ya Congo limesema miili ya watu 26 waliouawa katika shambulio lililofanywa na waasi mapema mwezi huu, imegunduliwa mashariki mwa nchi hiyo.
DRC Congo
Marehemu wote hao ambao walikuwa ni raia isipokuwa mmoja, walishambuliwa katika eneo la Beni katika jimbo la Kivu kaskazini wakati wakisafiri na gari ndogo ya kukodi

Mamlaka nchini humo zinasema kwamba zilishindwa kujua zilipo maiti hizo mapema kwa sababu ya mapigano makali yaliyokuwa yakitokea katika eneo hilo, ambako mamia ya watu waliuawa katika siku za hivi karibuni

Jeshi la Congo na Walinda amani wa Umoja wa Mataifa wamekuwa wakililaumu kundi la wapiganaji wa Uganda la Allied Democratic Forces ADF, kuhusika na mauaji hayo

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search