Mkurugenzi 'chupuchupu' jela miaka miwili..soma habari na Matukio360..share
Na
mwandishi wetu
GULAMABBAS
Murtaza (47) ambaye ni mkurugenzi wa
kampuni ya Ideal Trading Ltd ya Temeke Chang'ombe
VETA jijini Dar es Salaam, amenusurika
kifungo cha miaka miwili jela baada ya kulipa faini ya milioni 26.
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu
Murtaza
amelipa kiasi hicho cha fedha na kukwepa kifungo baada ya kukubali mashtaka
mawili ya kuishi bila kibali na kujihusisha
na biashara nchini.
Leo
katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi amemuhukumu
mshtakiwa huyo kulipa milioni moja katika kosa la kuhishi bila kibali.
Pia amemuhukumu mshtakiwa huyo kulipa kiasi cha
milioni 25 kwa kujihusisha na biashara
kama mkurugenzi wa kampuni ya Ideal Trading Ltd iliyopo eneo la Chang'ombe bila
ya kuwa na kibali.
Mshtakiwa
hiyo alifanikiwa kulipa kiasi hicho cha fedha na kukwepa kifungo cha miaka
miwili jela.
Mshtakiwa
huyo akiwa raia wa India na mkazi
wa Kenya anadaiwa kufayafanya
makosa hayo Oktoba 12, 2017. Upande
wa mashtaka uliwakilishwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka Wa Uhamiaji,
Novertus Mlay.
No comments:
Post a Comment