Naibu Waziri awabana Madiwani...soma habari kamili na Matukio360...#share
Na Mwandishi
wetu
NAIBU Waziri
wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Elias Kwandikwa amewataka madiwani kuanisha vipaumbele vyao vya barabara ili
ziingizwe kiurahisi kwenye mpango wa matengenezo.
Meneja
wa Wakala wa Barabara (TANROADS), mkoa wa Tabora Eng. Damian Ndibalinze akitoa
taarifa ya mradi kwa Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya
Ujenzi) Elias Kwandikwa, alipokagua ujenzi wa barabara ya Kaliua-Urambo km 28 kwa kiwango cha lami, mkoani humo. Kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe.
Aggrey Mwamri,
Ametoa wito huo leo mkoani Tabora alipokuwa akikagua ujenzi wa barabara ya
Kaliua-Urambo yenye urefu wa km 28 na kuwa mapendekezo yao yawasilishwe katika kamati za
maendeleo za wilaya, mikoa na bodi za barabara.
"Diwani analalamika kwamba barabara haijatengenezwa ama haifikiliwi kutengenezwa lakini ukifuatilia hakuna mahali popote ambapo taariza za barabara hiyo kutengenezwa zimewasilishwa", amesema Kwandikwa.
"Diwani analalamika kwamba barabara haijatengenezwa ama haifikiliwi kutengenezwa lakini ukifuatilia hakuna mahali popote ambapo taariza za barabara hiyo kutengenezwa zimewasilishwa", amesema Kwandikwa.
Amesisitiza umuhimu wa kupeleka mapendekezo hayo
kutasaidia barabara hizo kutambulika na kuondoa malalamiko kwa wananchi na
baadhi ya viongozi kwa kuwa zitaingizwa katika mipango ya ujenzi kwa wakati.
Kuhusu barabara hiyo ya Kaliua-Urambo inayojengwa kufuatia agizo la Rais Dkt John Magufuli, Kwandikwa amemtaka mkandarasi kuhakikisha ujenzi huo unafanyika kwa kuzingatia viwango vya ubora uliopangwa kwa mujibu wa mkataba wake.
Kuhusu barabara hiyo ya Kaliua-Urambo inayojengwa kufuatia agizo la Rais Dkt John Magufuli, Kwandikwa amemtaka mkandarasi kuhakikisha ujenzi huo unafanyika kwa kuzingatia viwango vya ubora uliopangwa kwa mujibu wa mkataba wake.
"Lengo
la mheshimiwa rais ni kurahisha huduma ya usafiri na usafirishaji kwa wananchi
hivyo mkandarasi huna budi kufanya kazi hii haraka na kwa kuzingatia
makubaliano ya mkataba wako.’ amesema waziri kwandika.
Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Aggrey Mwanri amemuhakikishia naibu waziri Kwandikwa kuwa serikali ya mkoa huo imejipanga kushirikiana na mkandarasi ili barabara hiyo ikamilike ndani ya muda uliopangwa.
Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Aggrey Mwanri amemuhakikishia naibu waziri Kwandikwa kuwa serikali ya mkoa huo imejipanga kushirikiana na mkandarasi ili barabara hiyo ikamilike ndani ya muda uliopangwa.
“Kwanza sisi kama mkoa tunamshukuru Rais kwa kuona umuhimu wa kutuwekea lami katika barabara hii kwa sababu itaongeza ufanisi kwa wananchi kufanya shughuli zao kiurahisi”, amesema Mwanri.
Naye Meneja wa Wakala wa Barabara (TANROADS), mkoa wa Tabora Eng. Damian Ndibalinze amesema kuwa Wakala utawasimamia makandarasi wazawa Samota Construction, Anam Roads Works na Jossam Contractor (JV) ili kuhakikisha wanamaliza ujenzi huo kwa wakati baada ya changamoto ya tatizo la maji kupatiwa ufumbuzi.
Naibu Waziri Mhe. Elias Kwandikwa, yupo katika ziara ya kikazi ya kukagua ujenzi wa barabara na madaraja katika mikoa ya Singida, Tabora na Kigoma.
No comments:
Post a Comment