Nyalandu ajiuzulu Ubunge, ang'atuka CCM kujiunga CHADEMA...soma habari kamili na Matukio360..#share
Na
Mwandishi wetu
MBUNGE
wa Singida Kaskazini Lazaro Nyalandu amejiuzulu
ubunge, nafasi zake zote CCM na ameomba kujiunga na CHADEMA
Lazaro Nyalandu
Leo
jijini Arusha akitangaza uamuzi huo, Nyalandu amesema ‘nimeamua kujiuzulu
nafasi yangu ya Ujumbe wa Halmashauri
Kuu ya Chama Cha Mapinduzi CCM, pamoja na nafasi zote za Uongozi ndani ya Chama
kuanzia leo, Oktoba 30, 2017.
‘Halikadhalika,
asubuhi ya leo nimemwandikia Spika wa Bunge,Job Ndugai, Mb., barua ya kujiuzulu
nafasi yangu ya UBUNGE wa Jimbo la Singida Kaskazini kupitia tiketi ya CCM,
nafasi ambayo nimeitumikia kwa vipindi vinne mfululizo tangu nilipochaguliwa kwa
mara ya kwanza mnamo mwaka 2000 hadi Sasa.’
Amesema
uamuzi wake huo ni kutoridhishwa na mwenendo wa hali ya kisiasa nchini, ikiwa
ni pamoja na ukiukwaji wa haki za kibinadamu, ongezeko la vitendo vya dhuluma
wanavyofanyiwa baadhi ya watanzania wenzetu, na kutokuwepo kwa mipaka ya wazi
kati ya MIHIMILI ya dola (Serikali, Bunge, na Mahakama) kunakofanya utendaji
kazi wa Kibunge wa Kutunga Sheria na wa Kuisimamia Serikali kutokuwa na uhuru
uliainishwa na kuwekwa bayana KIKATIBA.
VILEVILE,
Naamini kwamba bila Tanzania kupata Katiba Mpya Sasa, hakuna namna yeyote ya
kuifanya mihimili ya dola isiingiliane na kuwepo kwa ukomo wa wazi na
kujitegemea kwa dhahiri kwa mihimili ya Serikali, Bunge na mahakama ambayo ndio
chimbuko la Uongozi Bora wa nchi, na kuonesha kwa uwazi kuwa madaraka yote
yatokana na wananchi wenyewe, na kwamba Serikali ni ya Watu kwajili ya Watu.
MIMI
Naondoka na kukiacha Chama Cha Mapinduzi CCM, nikiwa nimekitumikia kuanzia
ngazi ya Uenyekiti wa UVCCM Mkoa, Ujumbe wa Kamati za Siasa Wilaya na Mkoa,
Ujumbe wa Kamati ya Wabunge Wote wa CCM na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM
TAIFA, kwani nimejiridhisha kuwa kwa
mwenendo wa hali ya kisiasa, kiuongozi na kiuchumi uliyopo Tanzania Sasa, CCM imepoteza
mwelekeo wake wa kuisimamia Serikali kama ilivyokuwa hapo awali. AIDHA, Naamini
kuwa, kama ilivyotokea kwa mihimili ya Bunge na Mahakama kutokuwa na uhuru
kamili, bila kuingiliwa kiutendaji kwa namna Moja au nyigine, CCM nayo imekuwa
Chini ya miguu ya dola badala ya chama kushika hatamu na kuikosoa Serikali
inapobidi kama yalivyokuwa maono ya Baba wa TAIFA MWALIMU Julius Kambarage
Nyerere.
Hivyo
basi, kwa dhamira yangu, na kwa uamuzi wangu mwenyewe, nikiwa na haki ya
KIKATIBA, natangaza KUKIHAMA Chama Cha Mapinduzi CCM leo hii, na nitaomba
IKIWAPENDEZA wanachama wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA, basi
waniruhusu kuingia MALANGONI mwao, niwe mwanachama, ili kuungana na CHADEMA na
watanzania wote wanaopenda kuleta mabadiliko ya kisiasa na kiuchumi nchini kwa
kupitia mfumo wa ki demokrasia na uhuru wa mawazo.
VILEVILE,
nimemua kujiuzulu KITI Cha Ubunge, Jimbo la Singida Kaskazini kuruhusu
kufanyika kwa UCHAGUZI mwingine ili wananchi wapate fursa ya kuchagua ITIKADI
wanayoona inawafaa kwa majira na nyakati hizi zenye changamoto lukuki nchini
Tanzania. Ni imani yangu, kamwe hayatakuwa ya bure maneno haya, wala uamuzi huu
niufanyao mbele ya Watanzania leo ili kwamba, SOTE kama TAIFA tuingie kwenye
mjadala wa kuijenga upya misingi ya nchi yetu. Ni maombi yangu kwa MUNGU kuwa
Haki itamalaki Tanzania. Upendo, amani na mshikamano wa watu wa imani zote za dini, mitazamo yote
ya kiitikadi za Kisiasa, na makabila yote nchini uimarike. Tushindane kisera na
kuruhusu tofauti za mawazo, lakini tubaki kama ndugu, na TAIFA lililo imara na
nchi yenye MAADILI.
No comments:
Post a Comment