Mourinho aendeleza tambo Liverpool vs Manchester United...soma habari kamili na Matukio360..#share
Klabu hizo mbili ni mahasimu wakuu na
United wanaweza kuwa alama 10 mbele ya Liverpool iwapo watashinda mechi hiyo ya
Jumamosi.
"Tunajua jinsi mashabiki wao
waliovyo na uadui dhidi yetu kihistoria, lakini hilo ndilo tunataka,"
Mourinho amesema.
"Sijawahi kumuona mchezaji
akilalamika 'oh, mazingira yalikuwa mabaya sana'."
"Huwa tunalalamika mashabiki
wakiwa kimya. Ni jambo la kupendeza kuchezea Anfield. Jambo la kupendeza."
Meneja wa Liverpool Jurgen Klopp atakuwa
akiadhimisha miaka miwili Liverpool wikendi hii na atakuwa bila mchezaji wake
nyota Sadio Mane.
Mane aliumia misuli ya paja akichezea
Senegal mechi za kufuzu Kombe la Dunia lakini Klopp anaamini wanaweza kujimudu
bila yeye.
"Bila shaka bado tunaweza kucheza
soka bila Sadio kama tulivyofanya awali - zaidi ya jinsi tulivyotaka,"
amesema Klopp. "Yeye ndiye mchezaji bora zaidi wetu na ana mkosi sana
kuumia.
"Wachezaji wengi wa timu mbalimbali
wametoka kuchezea timu za taifa na majeraha - ni tatizo kubwa kutokana na
mabadiliko ya mtindo wa mazoezi na uchezaji pia."
"Tunaweza kucheza bila yeye ingawa
tungependa sana kuwa na yeye kikosini.
Coutinho
kucheza
Liverpool watakuwa bila Mane
anayetarajiwa kukaa nje wiki sita, lakini Philippe Coutinho na Roberto Firmino
wanatarajiwa kuwepo hata baada ya safari ndefu ya kucheza mechi Brazil.
Kiungo wa kati wa Manchester United
Marouane Fellaini anatarajiwa kutocheza baada ya kuumia kano za goti akichezea
Ubelgiji. Nahodha Michael Carrick pia bado anauguza jeraha




No comments:
Post a Comment