Wizara yaomba radhi...soma habari kamili na Matukio360...#share


WIZARA ya Nishati imeomba radhi kufuatia hatua yake ya  kuahirisha mnada wa madini ya Tanzanite uliokuwa ufanyike katika mji mdogo wa Mererani Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara kuanzia Oktoba 12 hadi 15, 2017.


Waziri wa madini Angela Kairuki
Taarifa kwa vyombo vya habari kutoka kitengo cha mawasiliano Serikalini inasema “Wizara ya Madini inawaomba radhi wadau  wote wa sekta hii ndogo ya madini na vito hususan Tanzanite ambao wameathirika kwa namna moja au nyingine kutokana na kuahirishwa ghafla kwa mnada huo.”

Taarifa hiyo imesema sababu za kuahirishwa ni kuridhia maombi ya wadau wa mnada walioomba kupata muda zaidi wa maandalizi ili wapate fursa ya kushiriki kwa wingi.

Pia uongozi wa Wizara na Mkoa upate muda zaidi wa kuandaa mazingira salama na bora zaidi ya kufanyia mnada huo katika mji wa Merereni.

Mnada huo umeahirishwa hadi hapo utapotangazwa




About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search