Wa-Oman 300 wawasili Zanzibar.. Soma habari kamili hapa Matukio360.. #share


UJUMBE wa watu 300 ambao wanamwakilisha mfalme wa Oman Sheikh Sultan Qabous bin Said umewasili mjini Zanzibar  kwa  kutumia  meli aina ya ‘ Fulk Al l Salamah' inayotumiwa na familia ya ufalme huo.
Meli ya mfalme wa Oman ikiwaimetia nanga katika Bandari ya Zanzibar
Ujumbe huo uliotoka Muscat Oman uliwasili katika bandari ya Malindi Alhamisi na kupokewa na makamu wa rais wa pili Seif Ali Idd ambaye aliandamana na mawaziri wanne.

Ujumbe huo wa Oman uliongozwa na waziri wa mafuta na gesi Mohammed Al-ramh.wa Oman uliongozwa na waziri wa mafuta na gesi Mohammed Al-ramh.

Ziara hiyo inalenga kuhimiza amani na umoja duniani.
Akizungumza katika hafla hiyo, waziri katika ofisi ya makamu wa rais wa pili Mohammed amesema  ziara hiyo ni muhimu kwa serikali ya Zanzibar.

Amesema kuwa inafungua ukurasa mpya kuhusu ushirikiano kati ya mataifa hayo mawili yalio na historia ndefu.

Waziri huyo amesema  ujumbe huo pia utapewa fursa ya kutembelea maeneo ya kihistoria na afisi za serikali ili kubadilishana mawazo kuhusu ukuwaji wa kiuchumi.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search