Msemaji mkuu wa Serikali atoa siri tano za mafanikio...soma habari kamili na Matukio360...#share

Na mwandishi wetu
Mkurugenzi wa Habari Maelezo na Msemaji wa Serikali, Dk Hassan Abbas ametoa siri tano za mafanikio kwa wanafunzi wa kidato cha nne 2017 wanaotarajia kufanya mtihani wa taifa mwishoni mwa mwezi huu.

Mkurugenzi wa Idara ya Habari Maelezo na Msemaji mkuu wa Serikali Dk Hassan Abass
Siri ya kwanza ni malengo ya pili malengo makubwa ya tatu nidhamu na kusimamia malengo,  ya nne ushirikiano na siri ya tano kumshirikisha Mungu kwenye shughuli zote hasa za masomo.

Dk Abbas  aliwaasa wanafunzi hao jana alipokuwa  mgeni rasmi katika maafari ya 33 ya mwaka 2017 ya wanafunzi  459 wa kidato cha nne katika shule ya Sekondari Jitegemee (JKT).

“Siri  tano za mafanikio ni  lazima  ujiwekea malengo hasa  makubwa, nidhamu, kujituma, kusimamia malengo yako, ushirikiano na kumshirikisha Mungu hasa katika masomo yao.”

Dk Abbas amesema mojawapo ya  changamoto inazoikabili shule hiyo vitabu vya kiada na ziada ameahidi kuwapelekea.

Aliwatunuku vyeti wanafunzi 459 kati yao wasichana 209 na wavulana 250. Ameahidi kuwa  balozi wa shule hiyo.

Akisoma risala kwa niaba ya wanafunzi wa kidato cha nne 2017, mwanafuzi Isihaka Jamal alimuomba Dk Abbas kubuni mfumo wa kuwawezesha wanafunzi kufika shuleni kwa wakati na kuepukana na changamoto zinazowakabili hasa wanafunzi wa kike.

Jamal alisema usafiri kwa wanafunzi hasa  wakike ni changsmoto kwa kuwa wengi wao wamekuwa wakijinasua na tatizo hilo la usafiri kwa kutafuta njia mbadala kwa kujiingiza katika mapenzi na madereva daladala, bodaboda na kupelea kupata mimba na magonjwa.
Pia alisema shule hiyo inakabiliwa na changamoto ya kuwa majengo mengi ambayo ni ya dhamani, yanahitaji ukarabati.

Mkuu wa Shule hiyo ya Sekondari ya Jitegemee(JKT), Luteni Kanali, Robert Kessy aliwaasa wanafunzi hao kuwa wao wamewaanda kwa kuwapatia elimu bora  na nidhamu waizingatie.
Aliwakumbusha wanafunzi hao kuwa kufika  kidato cha nne siyo wamemaliza masomo hiyo ni elimu  wanatakiwa kuhakikisha wansjiendeleza zaidi kwa kuwa elimu ndiyo ufunguo wa maisha yao.
Pia aliwaasa wajiepushe kujiingiza katika matukio ya uhalifu, matumizi ya dawa za kulevya na vitendo hatarishi

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search