Uteuzi wa Rais Mugabe WHO wapingwa...Soma habari kamili na Matukio360..#share

SHIRIKA la Afya Duniani (WHO) limesema linafikiria upya uamuzi wake wa kumteua Rais wa Zimbabwe Robert Mugabe kuwa balozi mwema wa shirika hilo.
Rais wa Zimbabwe Robert Mugabe

Hayo yamebainishwa na Kiongozi wa WHO, Tedros Adhanon Ghebreyesus.

Hatua hiyo inakuja kufuatia ukosoaji mkubwa kutoka kwa viongozi mbalimbali ulimwenguni, kutokana na uamuzi huo wa kumteuwa Mugabe  anayelaaniwa na watu wengi duniani.

Ghebreyesus, amesema kuwa atatoa taarifa mpya hivi karibuni kuhusiana na uamuzi huo.

Kwa upande wa serikali ya Uingereza ikizungumzia hatua ya WHO kumteua Mugabe kuwa balozi, imesema, imeshtushwa na kuvunjika moyo juu ya uteuzi huo.

Msemaji mjini London, ameleza kuwa bwana Mugabe anakabili vikwazo vya Marekani na Umoja wa Ulaya, na kuteuliwa kwake, kutaathiri kazi za WHO.

Akifafanua uamuzi wa uteuzi huo , Mkurugenzi mkuu mpya wa WHO, Dr Tedros Adhanom Ghebreyesus, alisifu namna Zimbabwe inavyozingatia afya ya umma.

Lakini wakosoaji wanasema katika kipindi cha miaka thelathini na saba ya utawala wa rais Mugabe, huduma za afya zimekuwa mbaya ambapo wahudumu wa afya wamekuwa hawalipwi mara kwa mara , na kumekuwa na ukosefu mkubwa wa dawa muhimu .

Dr .Tedros, ni raia wa Ethiopia ambaye ni Muafrika wa kwanza kuongoza shirika la W.H.O. na alichaguliwa kwa ajili ya kukabiliana na kile kilichoaminiwa kuwa ni kugeuzwa kwa shirika hilo kuwa la kisiasa.


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search